< Zaburi 30 >
1 Utenzi wa kuweka wakfu hekalu. Zaburi ya Daudi. Nitakutukuza wewe, Ee Bwana, kwa kuwa umeniinua kutoka vilindi, na hukuacha adui zangu washangilie juu yangu.
A Canticle Psalm. In dedication to the house of David. I will extol you, Lord, for you have sustained me, and you have not allowed my enemies to delight over me.
2 Ee Bwana, Mungu wangu, nilikuita unisaidie na wewe umeniponya.
O Lord my God, I have cried out to you, and you have healed me.
3 Ee Bwana, umenitoa Kuzimu, umeniokoa nisishuke kwenye shimo la mauti. (Sheol )
Lord, you led my soul away from Hell. You have saved me from those who descend into the pit. (Sheol )
4 Mwimbieni Bwana, enyi watakatifu wake; lisifuni jina lake takatifu.
Sing a psalm to the Lord, you his saints, and confess with remembrance of his holiness.
5 Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi, bali upendo wake hudumu siku zote. Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha, lakini asubuhi kukawa na furaha.
For wrath is in his indignation, and life is in his will. Toward evening, weeping will linger, and toward morning, gladness.
6 Nilipofanikiwa nilisema, “Sitatikiswa kamwe.”
But I have said in my abundance: “I will never be disturbed.”
7 Ee Bwana, uliponijalia, uliuimarisha mlima wangu, lakini ulipouficha uso wako nilifadhaika.
O Lord, in your will, you made virtue preferable to beauty for me. You turned your face away from me, and I became disturbed.
8 Kwako wewe, Ee Bwana, niliita, kwa Bwana niliomba rehema:
To you, Lord, I will cry out. And I will make supplication to my God.
9 “Kuna faida gani katika kuangamia kwangu? Katika kushuka kwangu shimoni? Je, mavumbi yatakusifu? Je, yatatangaza uaminifu wako?
What use would there be in my blood, if I descend into corruption? Will dust confess to you or announce your truth?
10 Ee Bwana, unisikie na kunihurumia, Ee Bwana, uwe msaada wangu.”
The Lord has heard, and he has been merciful to me. The Lord has become my helper.
11 Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza, ulinivua nguo za gunia ukanivika shangwe,
You have turned my mourning into gladness for me. You have cut off my sackcloth, and you have surrounded me with joy.
12 ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya. Ee Bwana Mungu wangu, nitakushukuru milele.
So then, may my glory sing to you, and may I not regret it. O Lord, my God, I will confess to you for eternity.