< Zaburi 30 >
1 Utenzi wa kuweka wakfu hekalu. Zaburi ya Daudi. Nitakutukuza wewe, Ee Bwana, kwa kuwa umeniinua kutoka vilindi, na hukuacha adui zangu washangilie juu yangu.
I will extol thee, O Jehovah, for thou have raised me up, and have not made my foes to rejoice over me.
2 Ee Bwana, Mungu wangu, nilikuita unisaidie na wewe umeniponya.
O Jehovah my God, I cried to thee, and thou have healed me.
3 Ee Bwana, umenitoa Kuzimu, umeniokoa nisishuke kwenye shimo la mauti. (Sheol )
O Jehovah, thou have brought up my soul from Sheol. Thou have kept me alive, that I should not go down to the pit. (Sheol )
4 Mwimbieni Bwana, enyi watakatifu wake; lisifuni jina lake takatifu.
Sing praise to Jehovah, O ye sanctified of his, and give thanks to his holiness.
5 Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi, bali upendo wake hudumu siku zote. Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha, lakini asubuhi kukawa na furaha.
For his anger is but for a moment. His favor is for a lifetime. Weeping may tarry for the night, but joy is in the morning.
6 Nilipofanikiwa nilisema, “Sitatikiswa kamwe.”
As for me, I said in my prosperity, I shall never be moved.
7 Ee Bwana, uliponijalia, uliuimarisha mlima wangu, lakini ulipouficha uso wako nilifadhaika.
Thou, Jehovah, of thy favor had made my mountain to stand strong. Thou hid thy face; I was troubled.
8 Kwako wewe, Ee Bwana, niliita, kwa Bwana niliomba rehema:
I cried to thee, O Jehovah, and to Jehovah I made supplication.
9 “Kuna faida gani katika kuangamia kwangu? Katika kushuka kwangu shimoni? Je, mavumbi yatakusifu? Je, yatatangaza uaminifu wako?
What profit is there in my blood when I go down to the pit? Shall the dust praise thee? Shall it declare thy truth?
10 Ee Bwana, unisikie na kunihurumia, Ee Bwana, uwe msaada wangu.”
Hear, O Jehovah, and have mercy upon me. Jehovah, be thou my helper.
11 Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza, ulinivua nguo za gunia ukanivika shangwe,
Thou have turned for me my mourning into dancing. Thou have loosed my sackcloth, and girded me with gladness,
12 ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya. Ee Bwana Mungu wangu, nitakushukuru milele.
to the end that my glory may sing praise to thee, and not be silent. O Jehovah my God, I will give thanks to thee forever.