< Zaburi 30 >

1 Utenzi wa kuweka wakfu hekalu. Zaburi ya Daudi. Nitakutukuza wewe, Ee Bwana, kwa kuwa umeniinua kutoka vilindi, na hukuacha adui zangu washangilie juu yangu.
Psalam. Pjesma za posvećenje Doma. Davidov. Veličam te, Jahve, jer si me izbavio i nisi dao da se raduju nada mnom dušmani.
2 Ee Bwana, Mungu wangu, nilikuita unisaidie na wewe umeniponya.
Jahve, Bože moj, zazvah te, i ti si me ozdravio;
3 Ee Bwana, umenitoa Kuzimu, umeniokoa nisishuke kwenye shimo la mauti. (Sheol h7585)
Jahve, izveo si mi dušu iz Podzemlja, na rubu groba ti si me oživio. (Sheol h7585)
4 Mwimbieni Bwana, enyi watakatifu wake; lisifuni jina lake takatifu.
Pjevajte Jahvi, vjernici njegovi, zahvaljujte svetom imenu njegovu!
5 Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi, bali upendo wake hudumu siku zote. Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha, lakini asubuhi kukawa na furaha.
Jer samo za tren traje srdžba njegova, a čitav život dobrota njegova. Večer donese suze, a jutro klicanje.
6 Nilipofanikiwa nilisema, “Sitatikiswa kamwe.”
U svojoj sreći rekoh: “Neću se pokolebati nikada!”
7 Ee Bwana, uliponijalia, uliuimarisha mlima wangu, lakini ulipouficha uso wako nilifadhaika.
Dobrotom si me, o Jahve, na goru nade postavio, ali čim lice sakriješ, sav se uplašim.
8 Kwako wewe, Ee Bwana, niliita, kwa Bwana niliomba rehema:
Tada, Jahve, zavapih k tebi i zazvah milosrđe Boga svojega:
9 “Kuna faida gani katika kuangamia kwangu? Katika kushuka kwangu shimoni? Je, mavumbi yatakusifu? Je, yatatangaza uaminifu wako?
“Kakva je korist od krvi moje, kakva korist da u grob siđem? Zar će te prašina slaviti, zar će naviještati vjernost tvoju?”
10 Ee Bwana, unisikie na kunihurumia, Ee Bwana, uwe msaada wangu.”
Slušaj, o Jahve, i smiluj se meni; Jahve, budi mi na pomoć!
11 Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza, ulinivua nguo za gunia ukanivika shangwe,
Okrenuo si moj plač u igranje, skinuo kostrijet s mene i opasao me radošću.
12 ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya. Ee Bwana Mungu wangu, nitakushukuru milele.
Zato ti pjeva duša moja i neće zamuknuti: Jahve, Bože moj, dovijeka ću te hvaliti!

< Zaburi 30 >