< Zaburi 3 >

1 Zaburi ya Daudi. Alipomkimbia mwanawe Absalomu. Ee Bwana, tazama adui zangu walivyo wengi! Ni wengi kiasi gani wanaoinuka dhidi yangu!
Gospode! kako je mnogo neprijatelja mojih! Mnogi ustaju na me.
2 Wengi wanasema juu yangu, “Mungu hatamwokoa.”
Mnogi govore za dušu moju: nema mu pomoæi od Boga.
3 Lakini wewe, Ee Bwana, ni ngao pande zote; umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.
Ali ti si, Gospode, štit koji me zaklanja, slava moja; ti podižeš glavu moju.
4 Ninamlilia Bwana kwa sauti kuu, naye ananijibu kutoka mlima wake mtakatifu.
Glasom svojim vièem ka Gospodu, i èuje me sa svete gore svoje.
5 Ninajilaza na kupata usingizi; naamka tena, kwa maana Bwana hunitegemeza.
Ja liježem, spavam i ustajem, jer me Gospod èuva.
6 Sitaogopa makumi elfu ya adui, wanaojipanga dhidi yangu kila upande.
Ne bojim se mnogo tisuæa naroda što sa svijeh strana navaljuje na me.
7 Ee Bwana, amka! Niokoe, Ee Mungu wangu! Wapige adui zangu wote kwenye taya, vunja meno ya waovu.
Ustani, Gospode! pomozi mi, Bože moj! jer ti udaraš po obrazu sve neprijatelje moje; razbijaš zube bezbožnicima.
8 Kwa maana wokovu watoka kwa Bwana. Baraka yako na iwe juu ya watu wako.
Od Gospoda je spasenje; neka bude na narodu tvom blagoslov tvoj!

< Zaburi 3 >