< Zaburi 3 >

1 Zaburi ya Daudi. Alipomkimbia mwanawe Absalomu. Ee Bwana, tazama adui zangu walivyo wengi! Ni wengi kiasi gani wanaoinuka dhidi yangu!
ダビデがその子アブサロムを避けてのがれたときの歌 主よ、わたしに敵する者のいかに多いことでしょう。わたしに逆らって立つ者が多く、
2 Wengi wanasema juu yangu, “Mungu hatamwokoa.”
「彼には神の助けがない」と、わたしについて言う者が多いのです。 (セラ)
3 Lakini wewe, Ee Bwana, ni ngao pande zote; umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.
しかし主よ、あなたはわたしを囲む盾、わが栄え、わたしの頭を、もたげてくださるかたです。
4 Ninamlilia Bwana kwa sauti kuu, naye ananijibu kutoka mlima wake mtakatifu.
わたしが声をあげて主を呼ばわると、主は聖なる山からわたしに答えられる。 (セラ)
5 Ninajilaza na kupata usingizi; naamka tena, kwa maana Bwana hunitegemeza.
わたしはふして眠り、また目をさます。主がわたしをささえられるからだ。
6 Sitaogopa makumi elfu ya adui, wanaojipanga dhidi yangu kila upande.
わたしを囲んで立ち構えるちよろずの民をもわたしは恐れない。
7 Ee Bwana, amka! Niokoe, Ee Mungu wangu! Wapige adui zangu wote kwenye taya, vunja meno ya waovu.
主よ、お立ちください。わが神よ、わたしをお救いください。あなたはわたしのすべての敵のほおを打ち、悪しき者の歯を折られるのです。
8 Kwa maana wokovu watoka kwa Bwana. Baraka yako na iwe juu ya watu wako.
救は主のものです。どうかあなたの祝福があなたの民の上にありますように。 (セラ)

< Zaburi 3 >