< Zaburi 3 >

1 Zaburi ya Daudi. Alipomkimbia mwanawe Absalomu. Ee Bwana, tazama adui zangu walivyo wengi! Ni wengi kiasi gani wanaoinuka dhidi yangu!
מזמור לדוד בברחו מפני אבשלום בנו יהוה מה רבו צרי רבים קמים עלי׃
2 Wengi wanasema juu yangu, “Mungu hatamwokoa.”
רבים אמרים לנפשי אין ישועתה לו באלהים סלה׃
3 Lakini wewe, Ee Bwana, ni ngao pande zote; umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.
ואתה יהוה מגן בעדי כבודי ומרים ראשי׃
4 Ninamlilia Bwana kwa sauti kuu, naye ananijibu kutoka mlima wake mtakatifu.
קולי אל יהוה אקרא ויענני מהר קדשו סלה׃
5 Ninajilaza na kupata usingizi; naamka tena, kwa maana Bwana hunitegemeza.
אני שכבתי ואישנה הקיצותי כי יהוה יסמכני׃
6 Sitaogopa makumi elfu ya adui, wanaojipanga dhidi yangu kila upande.
לא אירא מרבבות עם אשר סביב שתו עלי׃
7 Ee Bwana, amka! Niokoe, Ee Mungu wangu! Wapige adui zangu wote kwenye taya, vunja meno ya waovu.
קומה יהוה הושיעני אלהי כי הכית את כל איבי לחי שני רשעים שברת׃
8 Kwa maana wokovu watoka kwa Bwana. Baraka yako na iwe juu ya watu wako.
ליהוה הישועה על עמך ברכתך סלה׃

< Zaburi 3 >