< Zaburi 3 >

1 Zaburi ya Daudi. Alipomkimbia mwanawe Absalomu. Ee Bwana, tazama adui zangu walivyo wengi! Ni wengi kiasi gani wanaoinuka dhidi yangu!
Psaume de David, lorsqu'il fuyait de devant son fils Absalom. Seigneur, pourquoi ceux qui m'affligent se sont-ils multipliés? Combien se soulèvent contre moi!
2 Wengi wanasema juu yangu, “Mungu hatamwokoa.”
Combien disent à mon âme qu'il n'est point de salut pour elle! Interlude.
3 Lakini wewe, Ee Bwana, ni ngao pande zote; umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.
Mais toi, Seigneur, tu es mon appui et ma gloire; c'est toi qui relève ma tête.
4 Ninamlilia Bwana kwa sauti kuu, naye ananijibu kutoka mlima wake mtakatifu.
De ma voix, j'ai crié au Seigneur, et il m'a entendu du haut de sa montagne sainte. Interlude.
5 Ninajilaza na kupata usingizi; naamka tena, kwa maana Bwana hunitegemeza.
Et je me suis endormi d'un profond sommeil; je me suis réveillé, car le Seigneur me défendra.
6 Sitaogopa makumi elfu ya adui, wanaojipanga dhidi yangu kila upande.
Je ne craindrai pas la foule du peuple qui m'assiège de tous côtés;
7 Ee Bwana, amka! Niokoe, Ee Mungu wangu! Wapige adui zangu wote kwenye taya, vunja meno ya waovu.
Lève-toi, Seigneur; sauve-moi, mon Dieu! Car tu as frappé tous ceux qui m'ont poursuivi sans cause, et tu as broyé les dents des pécheurs.
8 Kwa maana wokovu watoka kwa Bwana. Baraka yako na iwe juu ya watu wako.
Le salut vient du Seigneur, et ta bénédiction est sur ton peuple.

< Zaburi 3 >