< Zaburi 3 >
1 Zaburi ya Daudi. Alipomkimbia mwanawe Absalomu. Ee Bwana, tazama adui zangu walivyo wengi! Ni wengi kiasi gani wanaoinuka dhidi yangu!
Chant de David. A l’occasion de sa fuite devant Absalon, son fils Yahweh, que mes ennemis sont nombreux! Quelle multitude se lève contre moi!
2 Wengi wanasema juu yangu, “Mungu hatamwokoa.”
Nombreux sont ceux qui disent à mon sujet: « Plus de salut pour lui auprès de Dieu! » — Séla.
3 Lakini wewe, Ee Bwana, ni ngao pande zote; umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.
Mais toi, Yahweh, tu es mon bouclier; tu es ma gloire, et tu relèves ma tête.
4 Ninamlilia Bwana kwa sauti kuu, naye ananijibu kutoka mlima wake mtakatifu.
De ma voix je crie vers Yahweh, et il me répond de sa montagne sainte. — Séla.
5 Ninajilaza na kupata usingizi; naamka tena, kwa maana Bwana hunitegemeza.
Je me suis couché et me suis endormi; je me suis réveillé, car Yahweh est mon soutien.
6 Sitaogopa makumi elfu ya adui, wanaojipanga dhidi yangu kila upande.
je ne crains pas devant le peuple innombrable, qui m’assiège de toutes parts.
7 Ee Bwana, amka! Niokoe, Ee Mungu wangu! Wapige adui zangu wote kwenye taya, vunja meno ya waovu.
Lève-toi, Yahweh! Sauve-moi, mon Dieu! Car tu frappes à la joue tous mes ennemis, tu brises les dents des méchants.
8 Kwa maana wokovu watoka kwa Bwana. Baraka yako na iwe juu ya watu wako.
A Yahweh le salut! Que ta bénédiction soit sur ton peuple! — Séla.