< Zaburi 3 >

1 Zaburi ya Daudi. Alipomkimbia mwanawe Absalomu. Ee Bwana, tazama adui zangu walivyo wengi! Ni wengi kiasi gani wanaoinuka dhidi yangu!
A psalm of David when fled he from before - Absalom son his. O Yahweh how! they are many opponents my many [people] [are] rising up on me.
2 Wengi wanasema juu yangu, “Mungu hatamwokoa.”
Many [people] [are] saying of self my there not [is] deliverance for him in God (Selah)
3 Lakini wewe, Ee Bwana, ni ngao pande zote; umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.
And you O Yahweh [are] a shield behind me honor my and [the one who] lifts up head my.
4 Ninamlilia Bwana kwa sauti kuu, naye ananijibu kutoka mlima wake mtakatifu.
Voice my to Yahweh I called out and he answered me from [the] mountain of holiness his (Selah)
5 Ninajilaza na kupata usingizi; naamka tena, kwa maana Bwana hunitegemeza.
I I lay down and I slept! I awoke for Yahweh he sustains me.
6 Sitaogopa makumi elfu ya adui, wanaojipanga dhidi yangu kila upande.
Not I will be afraid from ten thousands of people who all around they have taken a stand on me.
7 Ee Bwana, amka! Niokoe, Ee Mungu wangu! Wapige adui zangu wote kwenye taya, vunja meno ya waovu.
Arise! O Yahweh - save me O God my for you have struck all enemies my jaw [the] teeth of wicked [people] you have broken.
8 Kwa maana wokovu watoka kwa Bwana. Baraka yako na iwe juu ya watu wako.
[belongs] to Yahweh deliverance [is] towards people your blessing your (Selah)

< Zaburi 3 >