< Zaburi 3 >
1 Zaburi ya Daudi. Alipomkimbia mwanawe Absalomu. Ee Bwana, tazama adui zangu walivyo wengi! Ni wengi kiasi gani wanaoinuka dhidi yangu!
A Psalm of David, when he fled from Absalom his son. LORD, how are mine adversaries increased! many are they that rise up against me.
2 Wengi wanasema juu yangu, “Mungu hatamwokoa.”
Many there be which say of my soul, There is no help for him in God. (Selah)
3 Lakini wewe, Ee Bwana, ni ngao pande zote; umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.
But thou, O LORD, art a shield about me; my glory, and the lifter up of mine head.
4 Ninamlilia Bwana kwa sauti kuu, naye ananijibu kutoka mlima wake mtakatifu.
I cry unto the LORD with my voice, and he answereth me out of his holy hill. (Selah)
5 Ninajilaza na kupata usingizi; naamka tena, kwa maana Bwana hunitegemeza.
I laid me down and slept; I awaked; for the LORD sustaineth me.
6 Sitaogopa makumi elfu ya adui, wanaojipanga dhidi yangu kila upande.
I will not be afraid of ten thousands of the people, that have set themselves against me round about.
7 Ee Bwana, amka! Niokoe, Ee Mungu wangu! Wapige adui zangu wote kwenye taya, vunja meno ya waovu.
Arise, O LORD; save me, O my God: for thou hast smitten all mine enemies upon the cheek bone; thou hast broken the teeth of the wicked.
8 Kwa maana wokovu watoka kwa Bwana. Baraka yako na iwe juu ya watu wako.
Salvation belongeth unto the LORD: thy blessing be upon thy people. (Selah)