< Zaburi 3 >

1 Zaburi ya Daudi. Alipomkimbia mwanawe Absalomu. Ee Bwana, tazama adui zangu walivyo wengi! Ni wengi kiasi gani wanaoinuka dhidi yangu!
“A psalm of David, when he fled from before Abshalom his son.” Lord, how numerous are my assailants! how many, that rise up against me!
2 Wengi wanasema juu yangu, “Mungu hatamwokoa.”
Many say of my soul, There is no help for him with God. (Selah)
3 Lakini wewe, Ee Bwana, ni ngao pande zote; umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.
But thou, O Lord, art a shield around me, my glory, and he that lifteth up my head.
4 Ninamlilia Bwana kwa sauti kuu, naye ananijibu kutoka mlima wake mtakatifu.
With my voice I call unto the Lord, and he answereth me out of his holy mountain. (Selah)
5 Ninajilaza na kupata usingizi; naamka tena, kwa maana Bwana hunitegemeza.
I laid myself down and slept: I awoke; for the Lord sustaineth me.
6 Sitaogopa makumi elfu ya adui, wanaojipanga dhidi yangu kila upande.
I will not be afraid of ten thousands of people, that have placed themselves round about against me.
7 Ee Bwana, amka! Niokoe, Ee Mungu wangu! Wapige adui zangu wote kwenye taya, vunja meno ya waovu.
Arise, O Lord, help me, O my God; for thou smitest all my enemies upon the cheek bone: the teeth of the wicked dost thou break.
8 Kwa maana wokovu watoka kwa Bwana. Baraka yako na iwe juu ya watu wako.
Salvation belongeth unto the Lord: thy blessing be upon thy people. (Selah)

< Zaburi 3 >