< Zaburi 3 >

1 Zaburi ya Daudi. Alipomkimbia mwanawe Absalomu. Ee Bwana, tazama adui zangu walivyo wengi! Ni wengi kiasi gani wanaoinuka dhidi yangu!
The psalm of David when he fled from the face of his son Absalom. Why, O Lord, are they multiplied that afflict me? many are they who rise up against me.
2 Wengi wanasema juu yangu, “Mungu hatamwokoa.”
Many say to my soul: There is no salvation for him in his God.
3 Lakini wewe, Ee Bwana, ni ngao pande zote; umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.
But thou, O Lord art my protector, my glory, and the lifter up of my head.
4 Ninamlilia Bwana kwa sauti kuu, naye ananijibu kutoka mlima wake mtakatifu.
I have cried to the Lord with my voice: and he hath heard me from his holy hill.
5 Ninajilaza na kupata usingizi; naamka tena, kwa maana Bwana hunitegemeza.
I have slept and taken my rest: and I have risen up, because the Lord hath protected me.
6 Sitaogopa makumi elfu ya adui, wanaojipanga dhidi yangu kila upande.
I will not fear thousands of the people, surrounding me: arise, O Lord; save me, O my God.
7 Ee Bwana, amka! Niokoe, Ee Mungu wangu! Wapige adui zangu wote kwenye taya, vunja meno ya waovu.
For thou hast struck all them who are my adversaries without cause: thou hast broken the teeth of sinners.
8 Kwa maana wokovu watoka kwa Bwana. Baraka yako na iwe juu ya watu wako.
Salvation is of the Lord: and thy blessing is upon thy people.

< Zaburi 3 >