< Zaburi 3 >

1 Zaburi ya Daudi. Alipomkimbia mwanawe Absalomu. Ee Bwana, tazama adui zangu walivyo wengi! Ni wengi kiasi gani wanaoinuka dhidi yangu!
A Psalm of David. When he fled from the face of his son, Absalom. Lord, why have those who trouble me been multiplied? Many rise up against me.
2 Wengi wanasema juu yangu, “Mungu hatamwokoa.”
Many say to my soul, “There is no salvation for him in his God.” (Pause)
3 Lakini wewe, Ee Bwana, ni ngao pande zote; umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.
But you, Lord, are my supporter, my glory, and the one who raises up my head.
4 Ninamlilia Bwana kwa sauti kuu, naye ananijibu kutoka mlima wake mtakatifu.
I have cried out to the Lord with my voice, and he has heard me from his holy mountain. (Pause)
5 Ninajilaza na kupata usingizi; naamka tena, kwa maana Bwana hunitegemeza.
I have slept, and I have been stupefied. But I awakened because the Lord has taken me up.
6 Sitaogopa makumi elfu ya adui, wanaojipanga dhidi yangu kila upande.
I will not fear the thousands of people surrounding me. Rise up, Lord. Save me, my God.
7 Ee Bwana, amka! Niokoe, Ee Mungu wangu! Wapige adui zangu wote kwenye taya, vunja meno ya waovu.
For you have struck all those who oppose me without cause. You have broken the teeth of sinners.
8 Kwa maana wokovu watoka kwa Bwana. Baraka yako na iwe juu ya watu wako.
Salvation is of the Lord, and your blessing is upon your people. (Pause)

< Zaburi 3 >