< Zaburi 3 >
1 Zaburi ya Daudi. Alipomkimbia mwanawe Absalomu. Ee Bwana, tazama adui zangu walivyo wengi! Ni wengi kiasi gani wanaoinuka dhidi yangu!
A Psalm of David, when he fled from the presence of his son Abessalom. O Lord, why are they that afflict me multiplied? many rise up against me.
2 Wengi wanasema juu yangu, “Mungu hatamwokoa.”
Many say concerning my soul, There is no deliverance for him in his God. (Pause)
3 Lakini wewe, Ee Bwana, ni ngao pande zote; umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.
But you, O Lord, are my helper: my glory, and the one that lifts up my head.
4 Ninamlilia Bwana kwa sauti kuu, naye ananijibu kutoka mlima wake mtakatifu.
I cried to the Lord with my voice, and he heard me out of his holy mountain. (Pause)
5 Ninajilaza na kupata usingizi; naamka tena, kwa maana Bwana hunitegemeza.
I lay down and slept; I awaked; for the Lord will help me.
6 Sitaogopa makumi elfu ya adui, wanaojipanga dhidi yangu kila upande.
I will not be afraid of ten thousands of people, who beset me round about.
7 Ee Bwana, amka! Niokoe, Ee Mungu wangu! Wapige adui zangu wote kwenye taya, vunja meno ya waovu.
Arise, Lord; deliver me, my God: for you have struck all who were without cause mine enemies; you have broken the teeth of sinners.
8 Kwa maana wokovu watoka kwa Bwana. Baraka yako na iwe juu ya watu wako.
Deliverance is the Lord's, and your blessing is upon your people.