< Zaburi 29 >
1 Zaburi ya Daudi. Mpeni Bwana, enyi mashujaa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
En psalm av David. Given åt HERREN, I Guds sönder, given åt HERREN ära och makt;
2 Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.
given åt HERREN hans namns ära, tillbedjen HERREN i helig skrud.
3 Sauti ya Bwana iko juu ya maji; Mungu wa utukufu hupiga radi, Bwana hupiga radi juu ya maji makuu.
HERRENS röst går ovan vattnen; Gud, den härlige, dundrar, ja, HERREN, ovan de stora vattnen.
4 Sauti ya Bwana ina nguvu; sauti ya Bwana ni tukufu.
HERRENS röst ljuder med makt, HERRENS röst ljuder härligt.
5 Sauti ya Bwana huvunja mierezi; Bwana huvunja vipande vipande mierezi ya Lebanoni.
HERRENS röst bräcker cedrar, HERREN bräcker Libanons cedrar.
6 Hufanya Lebanoni irukaruke kama ndama, Sirioni urukaruke kama mwana nyati.
Han kommer dem att hoppa likasom kalvar, Libanon och Sirjon såsom unga vildoxar.
7 Sauti ya Bwana hupiga kwa miali ya umeme wa radi.
HERRENS röst sprider ljungeldslågor.
8 Sauti ya Bwana hutikisa jangwa; Bwana hutikisa Jangwa la Kadeshi.
HERRENS röst kommer öknen att bäva, HERREN kommer Kades' öken att bäva.
9 Sauti ya Bwana huzalisha ayala, na huuacha msitu wazi. Hekaluni mwake wote wasema, “Utukufu!”
HERRENS röst bringar hindarna att föda; skogarnas klädnad rycker den bort. I hans himmelska boning förkunnar allting hans ära.
10 Bwana huketi akiwa ametawazwa juu ya gharika; Bwana ametawazwa kuwa Mfalme milele.
HERREN på sin tron bjöd floden komma, och HERREN tronar såsom konung evinnerligen.
11 Bwana huwapa watu wake nguvu; Bwana huwabariki watu wake kwa kuwapa amani.
HERREN skall giva makt åt sitt folk, HERREN skall välsigna sitt folk med frid.