< Zaburi 29 >

1 Zaburi ya Daudi. Mpeni Bwana, enyi mashujaa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
Psalm Dawidowy. Oddawajcie Panu synowie mocarzów, oddawajcie Panu chwałę i moc.
2 Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.
Oddawajcie Panu chwałę imienia jego; kłaniajcie się Panu w ozdobie świętobliwości.
3 Sauti ya Bwana iko juu ya maji; Mungu wa utukufu hupiga radi, Bwana hupiga radi juu ya maji makuu.
Głos Pański nad wodami; Bóg chwalebny wzbudza gromy, Pan nad wodami wielkiemi.
4 Sauti ya Bwana ina nguvu; sauti ya Bwana ni tukufu.
Głos Pański mocny, głos Pański wielmożny,
5 Sauti ya Bwana huvunja mierezi; Bwana huvunja vipande vipande mierezi ya Lebanoni.
Głos Pański cedry łamie; kruszy Pan cedry Libańskie,
6 Hufanya Lebanoni irukaruke kama ndama, Sirioni urukaruke kama mwana nyati.
I czyni, że skaczą jako cielęta; Liban i Syryjon jako młody jednorożec.
7 Sauti ya Bwana hupiga kwa miali ya umeme wa radi.
Głos Pański krzesze płomień ognisty.
8 Sauti ya Bwana hutikisa jangwa; Bwana hutikisa Jangwa la Kadeshi.
Na głos Pański z bólem pustynia rodzą; z bólem rodzi na głos Pański pustynai Kades.
9 Sauti ya Bwana huzalisha ayala, na huuacha msitu wazi. Hekaluni mwake wote wasema, “Utukufu!”
Na głos Pański z bólem rodzą łanie, i odkrywają się lasy; ale w kościele swym opowiada wszystkę chwałę swoję.
10 Bwana huketi akiwa ametawazwa juu ya gharika; Bwana ametawazwa kuwa Mfalme milele.
Pan nad potopem siedział, i będzie siedział Pan, będąc królem na wieki.
11 Bwana huwapa watu wake nguvu; Bwana huwabariki watu wake kwa kuwapa amani.
Pan doda mocy ludowi swojemu; Pan będzie błogosławił ludowi swemu w pokoju.

< Zaburi 29 >