< Zaburi 29 >

1 Zaburi ya Daudi. Mpeni Bwana, enyi mashujaa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
A Psalm by David. Ascribe to Yahweh, you sons of the mighty, ascribe to Yahweh glory and strength.
2 Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.
Ascribe to Yahweh the glory due to his name. Worship Yahweh in holy array.
3 Sauti ya Bwana iko juu ya maji; Mungu wa utukufu hupiga radi, Bwana hupiga radi juu ya maji makuu.
Yahweh’s voice is on the waters. The God of glory thunders, even Yahweh on many waters.
4 Sauti ya Bwana ina nguvu; sauti ya Bwana ni tukufu.
Yahweh’s voice is powerful. Yahweh’s voice is full of majesty.
5 Sauti ya Bwana huvunja mierezi; Bwana huvunja vipande vipande mierezi ya Lebanoni.
Yahweh’s voice breaks the cedars. Yes, Yahweh breaks in pieces the cedars of Lebanon.
6 Hufanya Lebanoni irukaruke kama ndama, Sirioni urukaruke kama mwana nyati.
He makes them also to skip like a calf; Lebanon and Sirion like a young, wild ox.
7 Sauti ya Bwana hupiga kwa miali ya umeme wa radi.
Yahweh’s voice strikes with flashes of lightning.
8 Sauti ya Bwana hutikisa jangwa; Bwana hutikisa Jangwa la Kadeshi.
Yahweh’s voice shakes the wilderness. Yahweh shakes the wilderness of Kadesh.
9 Sauti ya Bwana huzalisha ayala, na huuacha msitu wazi. Hekaluni mwake wote wasema, “Utukufu!”
Yahweh’s voice makes the deer calve, and strips the forests bare. In his temple everything says, “Glory!”
10 Bwana huketi akiwa ametawazwa juu ya gharika; Bwana ametawazwa kuwa Mfalme milele.
Yahweh sat enthroned at the Flood. Yes, Yahweh sits as King forever.
11 Bwana huwapa watu wake nguvu; Bwana huwabariki watu wake kwa kuwapa amani.
Yahweh will give strength to his people. Yahweh will bless his people with peace.

< Zaburi 29 >