< Zaburi 29 >

1 Zaburi ya Daudi. Mpeni Bwana, enyi mashujaa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
Give unto Yhwh, O ye mighty, give unto Yhwh glory and strength.
2 Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.
Give unto Yhwh the glory due unto his name; worship Yhwh in the beauty of holiness.
3 Sauti ya Bwana iko juu ya maji; Mungu wa utukufu hupiga radi, Bwana hupiga radi juu ya maji makuu.
The voice of Yhwh is upon the waters: the God of glory thundereth: Yhwh is upon many waters.
4 Sauti ya Bwana ina nguvu; sauti ya Bwana ni tukufu.
The voice of Yhwh is powerful; the voice of Yhwh is full of majesty.
5 Sauti ya Bwana huvunja mierezi; Bwana huvunja vipande vipande mierezi ya Lebanoni.
The voice of Yhwh breaketh the cedars; yea, Yhwh breaketh the cedars of Lebanon.
6 Hufanya Lebanoni irukaruke kama ndama, Sirioni urukaruke kama mwana nyati.
He maketh them also to skip like a calf; Lebanon and Sirion like a young unicorn.
7 Sauti ya Bwana hupiga kwa miali ya umeme wa radi.
The voice of Yhwh divideth the flames of fire.
8 Sauti ya Bwana hutikisa jangwa; Bwana hutikisa Jangwa la Kadeshi.
The voice of Yhwh shaketh the wilderness; Yhwh shaketh the wilderness of Kadesh.
9 Sauti ya Bwana huzalisha ayala, na huuacha msitu wazi. Hekaluni mwake wote wasema, “Utukufu!”
The voice of Yhwh maketh the hinds to calve, and discovereth the forests: and in his temple doth every one speak of his glory.
10 Bwana huketi akiwa ametawazwa juu ya gharika; Bwana ametawazwa kuwa Mfalme milele.
Yhwh sitteth upon the flood; yea, Yhwh sitteth King for ever.
11 Bwana huwapa watu wake nguvu; Bwana huwabariki watu wake kwa kuwapa amani.
Yhwh will give strength unto his people; Yhwh will bless his people with peace.

< Zaburi 29 >