< Zaburi 28 >

1 Zaburi ya Daudi. Ninakuita wewe, Ee Bwana, Mwamba wangu; usiwe kwangu kama kiziwi. Kwa sababu ukinyamaza nitafanana na walioshuka shimoni.
De David. Éternel! je crie à toi; mon rocher! ne te tais point envers moi; de peur que, si tu gardes le silence envers moi, je ne sois fait semblable à ceux qui descendent dans la fosse.
2 Sikia kilio changu unihurumie ninapokuita kwa ajili ya msaada, niinuapo mikono yangu kuelekea Patakatifu pa Patakatifu pako.
Écoute la voix de mes supplications quand je crie à toi, quand j’élève mes mains vers l’oracle de ta sainteté.
3 Usiniburute pamoja na waovu, pamoja na hao watendao mabaya, ambao huzungumza na jirani zao maneno mazuri, lakini mioyoni mwao wameficha chuki.
Ne m’entraîne pas avec les méchants, ni avec les ouvriers d’iniquité, qui parlent paix avec leur prochain, tandis que la méchanceté est dans leur cœur.
4 Walipe sawasawa na matendo yao, sawasawa na matendo yao maovu; walipe sawasawa na kazi za mikono yao, uwalipe wanavyostahili.
Donne-leur selon leur œuvre et selon l’iniquité de leurs actions; donne-leur selon l’ouvrage de leurs mains, rends-leur selon ce qu’ils ont fait.
5 Kwa kuwa hawaheshimu kazi za Bwana, na yale ambayo mikono yake imetenda, atawabomoa na kamwe hatawajenga tena.
Parce qu’ils ne discernent pas les œuvres de l’Éternel, ni l’ouvrage de ses mains, il les détruira et ne les édifiera point.
6 Bwana asifiwe, kwa maana amesikia kilio changu nikimwomba anihurumie.
Béni soit l’Éternel! car il a entendu la voix de mes supplications.
7 Bwana ni nguvu zangu na ngao yangu, moyo wangu umemtumaini yeye, nami nimesaidiwa. Moyo wangu unarukaruka kwa furaha nami nitamshukuru kwa wimbo.
L’Éternel est ma force et mon bouclier; en lui mon cœur a eu sa confiance, et j’ai été secouru; et mon cœur se réjouit, et je le célébrerai dans mon cantique.
8 Bwana ni nguvu ya watu wake, ngome ya wokovu kwa mpakwa mafuta wake.
L’Éternel est leur force, et il est le lieu fort des délivrances de son oint.
9 Waokoe watu wako na uubariki urithi wako; uwe mchungaji wao na uwabebe milele.
Sauve ton peuple, et bénis ton héritage; et pais-les, et élève-les pour toujours.

< Zaburi 28 >