< Zaburi 28 >
1 Zaburi ya Daudi. Ninakuita wewe, Ee Bwana, Mwamba wangu; usiwe kwangu kama kiziwi. Kwa sababu ukinyamaza nitafanana na walioshuka shimoni.
De David. C’est vers toi, Yahweh, que je crie; mon rocher, ne reste pas sourd à ma voix, de peur que, si tu gardes le silence, je ne ressemble à ceux qui descendent dans la fosse.
2 Sikia kilio changu unihurumie ninapokuita kwa ajili ya msaada, niinuapo mikono yangu kuelekea Patakatifu pa Patakatifu pako.
Écoute la voix de mes supplications, quand je crie vers toi, quand j’élève mes mains vers ton saint sanctuaire.
3 Usiniburute pamoja na waovu, pamoja na hao watendao mabaya, ambao huzungumza na jirani zao maneno mazuri, lakini mioyoni mwao wameficha chuki.
Ne m’emporte pas avec les méchants et les artisans d’iniquité, qui parlent de paix à leur prochain, et qui ont la malice dans le cœur.
4 Walipe sawasawa na matendo yao, sawasawa na matendo yao maovu; walipe sawasawa na kazi za mikono yao, uwalipe wanavyostahili.
Rends-leur selon leurs œuvres, et selon la malice de leurs actions; rends-leur selon l’ouvrage de leurs mains, donne-leur le salaire qu’ils méritent.
5 Kwa kuwa hawaheshimu kazi za Bwana, na yale ambayo mikono yake imetenda, atawabomoa na kamwe hatawajenga tena.
Car ils ne prennent pas garde aux œuvres de Yahweh, à l’ouvrage de ses mains: il les détruira et ne les bâtira pas.
6 Bwana asifiwe, kwa maana amesikia kilio changu nikimwomba anihurumie.
Béni soit Yahweh, car il a entendu la voix de mes supplications!
7 Bwana ni nguvu zangu na ngao yangu, moyo wangu umemtumaini yeye, nami nimesaidiwa. Moyo wangu unarukaruka kwa furaha nami nitamshukuru kwa wimbo.
Yahweh est ma force et mon bouclier; en lui s’est confié mon cœur. J’ai été secouru; aussi mon cœur est dans l’allégresse, et je le louerai par mes cantiques.
8 Bwana ni nguvu ya watu wake, ngome ya wokovu kwa mpakwa mafuta wake.
Yahweh est la force de son peuple, il est une forteresse de salut pour son Oint.
9 Waokoe watu wako na uubariki urithi wako; uwe mchungaji wao na uwabebe milele.
Sauve ton peuple et bénis ton héritage! Sois leur pasteur et porte-les à jamais!