< Zaburi 28 >

1 Zaburi ya Daudi. Ninakuita wewe, Ee Bwana, Mwamba wangu; usiwe kwangu kama kiziwi. Kwa sababu ukinyamaza nitafanana na walioshuka shimoni.
[A Psalm] of David. To thee will I cry, O LORD my rock; be not silent to me: lest, [if] thou shouldst be silent to me, I should become like them that go down into the pit.
2 Sikia kilio changu unihurumie ninapokuita kwa ajili ya msaada, niinuapo mikono yangu kuelekea Patakatifu pa Patakatifu pako.
Hear the voice of my supplications, when I cry to thee, when I lift my hands towards thy holy oracle.
3 Usiniburute pamoja na waovu, pamoja na hao watendao mabaya, ambao huzungumza na jirani zao maneno mazuri, lakini mioyoni mwao wameficha chuki.
Draw me not away with the wicked, and with the workers of iniquity, who speak peace to their neighbors, but mischief [is] in their hearts.
4 Walipe sawasawa na matendo yao, sawasawa na matendo yao maovu; walipe sawasawa na kazi za mikono yao, uwalipe wanavyostahili.
Give them according to their deeds, and according to the wickedness of their endeavors: give them after the work of their hands; render to them their desert.
5 Kwa kuwa hawaheshimu kazi za Bwana, na yale ambayo mikono yake imetenda, atawabomoa na kamwe hatawajenga tena.
Because they regard not the works of the LORD, nor the operation of his hands, he will destroy them, and not build them up.
6 Bwana asifiwe, kwa maana amesikia kilio changu nikimwomba anihurumie.
Blessed [be] the LORD, because he hath heard the voice of my supplications.
7 Bwana ni nguvu zangu na ngao yangu, moyo wangu umemtumaini yeye, nami nimesaidiwa. Moyo wangu unarukaruka kwa furaha nami nitamshukuru kwa wimbo.
The LORD [is] my strength, and my shield; my heart trusted in him, and I am helped: therefore my heart greatly rejoiceth; and with my song will I praise him.
8 Bwana ni nguvu ya watu wake, ngome ya wokovu kwa mpakwa mafuta wake.
The LORD [is] their strength, and he [is] the saving strength of his anointed.
9 Waokoe watu wako na uubariki urithi wako; uwe mchungaji wao na uwabebe milele.
Save thy people, and bless thy inheritance: feed them also, and lift them up for ever.

< Zaburi 28 >