< Zaburi 28 >
1 Zaburi ya Daudi. Ninakuita wewe, Ee Bwana, Mwamba wangu; usiwe kwangu kama kiziwi. Kwa sababu ukinyamaza nitafanana na walioshuka shimoni.
Of David. Unto you, O Lord, do I cry; my rock, be not deaf to me: lest, through holding your peace, I become like those who go down to the pit.
2 Sikia kilio changu unihurumie ninapokuita kwa ajili ya msaada, niinuapo mikono yangu kuelekea Patakatifu pa Patakatifu pako.
Hear my loud entreaty, as I cry for help to you, lifting my hands, O Lord, towards your holy chancel.
3 Usiniburute pamoja na waovu, pamoja na hao watendao mabaya, ambao huzungumza na jirani zao maneno mazuri, lakini mioyoni mwao wameficha chuki.
Take me not off with the wicked, nor with the workers of wrong, whose speech to their neighbors is friendly, while evil is in their heart.
4 Walipe sawasawa na matendo yao, sawasawa na matendo yao maovu; walipe sawasawa na kazi za mikono yao, uwalipe wanavyostahili.
Give them as they have done, as their wicked deeds deserve. As their hands have wrought, so give to them: requite to them their deserts.
5 Kwa kuwa hawaheshimu kazi za Bwana, na yale ambayo mikono yake imetenda, atawabomoa na kamwe hatawajenga tena.
They are blind to all that the Lord does, to all that his hands have wrought; and so he will tear them down, to build them up no more.
6 Bwana asifiwe, kwa maana amesikia kilio changu nikimwomba anihurumie.
Blest be the Lord, who has heard my voice as I plead for mercy.
7 Bwana ni nguvu zangu na ngao yangu, moyo wangu umemtumaini yeye, nami nimesaidiwa. Moyo wangu unarukaruka kwa furaha nami nitamshukuru kwa wimbo.
The Lord is my strength and my shield; my heart trusts in him. I was helped: so my heart is exultant, and in my song I will praise him.
8 Bwana ni nguvu ya watu wake, ngome ya wokovu kwa mpakwa mafuta wake.
The Lord is the strength of his people, the fortress who saves his anointed.
9 Waokoe watu wako na uubariki urithi wako; uwe mchungaji wao na uwabebe milele.
O save your people, and bless your inheritance. Be their shepherd and carry them forever.