< Zaburi 28 >

1 Zaburi ya Daudi. Ninakuita wewe, Ee Bwana, Mwamba wangu; usiwe kwangu kama kiziwi. Kwa sababu ukinyamaza nitafanana na walioshuka shimoni.
“A psalm of David.” To thee do I cry, O LORD! O my rock! be not silent to me, Lest, if thou answer me not, I become like those who go down to the pit!
2 Sikia kilio changu unihurumie ninapokuita kwa ajili ya msaada, niinuapo mikono yangu kuelekea Patakatifu pa Patakatifu pako.
Hear the voice of my supplication, when I cry unto thee, When I lift up my hands to thy most holy sanctuary!
3 Usiniburute pamoja na waovu, pamoja na hao watendao mabaya, ambao huzungumza na jirani zao maneno mazuri, lakini mioyoni mwao wameficha chuki.
Draw me not away with the impious, and with evil-doers, Who speak peace to their neighbors, while mischief is in their hearts!
4 Walipe sawasawa na matendo yao, sawasawa na matendo yao maovu; walipe sawasawa na kazi za mikono yao, uwalipe wanavyostahili.
Give them according to their deeds, and the wickedness of their doings; Give them according to the work of their hands; Render to them their desert!
5 Kwa kuwa hawaheshimu kazi za Bwana, na yale ambayo mikono yake imetenda, atawabomoa na kamwe hatawajenga tena.
For they regard not the doings of the LORD, nor the work of his hands; Therefore will he destroy them, and not again build them up.
6 Bwana asifiwe, kwa maana amesikia kilio changu nikimwomba anihurumie.
Praised be the LORD, for he hath heard the voice of my supplications!
7 Bwana ni nguvu zangu na ngao yangu, moyo wangu umemtumaini yeye, nami nimesaidiwa. Moyo wangu unarukaruka kwa furaha nami nitamshukuru kwa wimbo.
The LORD is my strength and my shield; My heart trusteth in him, and he helpeth me; Therefore doth my heart exult, And in my song I will praise him.
8 Bwana ni nguvu ya watu wake, ngome ya wokovu kwa mpakwa mafuta wake.
Jehovah is the strength of his people; He is the protecting shield of his anointed.
9 Waokoe watu wako na uubariki urithi wako; uwe mchungaji wao na uwabebe milele.
Save thy people, and bless thine inheritance; Feed them also, and build them up for ever!

< Zaburi 28 >