< Zaburi 26 >

1 Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, nithibitishe katika haki, maana nimeishi maisha yasiyo na lawama; nimemtumainia Bwana bila kusitasita.
Davut'un mezmuru Beni haklı çıkar, ya RAB, Çünkü dürüst bir yaşam sürdüm; Sarsılmadan RAB'be güvendim.
2 Ee Bwana, unijaribu, unipime, uuchunguze moyo wangu na mawazo yangu;
Dene beni, ya RAB, sına; Duygularımı, düşüncelerimi yokla.
3 kwa maana upendo wako uko mbele yangu daima, nami natembea siku zote katika kweli yako.
Çünkü sevgini hep göz önünde tutuyor, Senin gerçeğini yaşıyorum ben.
4 Siketi pamoja na watu wadanganyifu, wala siandamani na wanafiki,
Yalancılarla oturmam, İkiyüzlülerin suyuna gitmem.
5 ninachukia kusanyiko la watenda mabaya na ninakataa kuketi pamoja na waovu.
Kötülük yapanlar topluluğundan nefret ederim, Fesatçıların arasına girmem.
6 Ninanawa mikono yangu kwa kuwa sina hatia, naikaribia madhabahu yako, Ee Bwana,
Suçsuzluğumu göstermek için ellerimi yıkar, Sunağının çevresinde dönerim, ya RAB,
7 nikitangaza sifa yako kwa sauti kubwa, huku nikisimulia matendo yako ya ajabu.
Yüksek sesle şükranımı duyurmak Ve bütün harikalarını anlatmak için.
8 Ee Bwana, naipenda nyumba yako mahali unakoishi, mahali ambapo utukufu wako hukaa.
Severim, ya RAB, yaşadığın evi, Görkeminin bulunduğu yeri.
9 Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda dhambi, wala uhai wangu pamoja na wamwagao damu,
Günahkârların, Eli kanlı adamların yanısıra canımı alma.
10 ambao mikononi mwao kuna mipango miovu, ambao mikono yao ya kuume imejaa rushwa.
Onların elleri kötülük aletidir, Sağ elleri rüşvet doludur.
11 Bali mimi ninaishi maisha yasiyo na lawama; nikomboe na unihurumie.
Ama ben dürüst yaşarım, Kurtar beni, lütfet bana!
12 Miguu yangu imesimama katika uwanja tambarare; katika kusanyiko kuu nitamsifu Bwana.
Ayağım emin yerde duruyor. Topluluk içinde sana övgüler sunacağım, ya RAB.

< Zaburi 26 >