< Zaburi 26 >

1 Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, nithibitishe katika haki, maana nimeishi maisha yasiyo na lawama; nimemtumainia Bwana bila kusitasita.
Defiéndeme, oh Yavé, porque en mi integridad anduve, Y en Yavé confié sin titubear.
2 Ee Bwana, unijaribu, unipime, uuchunguze moyo wangu na mawazo yangu;
Examíname, oh Yavé, y pruébame. Escudriña lo más íntimo de mi personalidad y mi corazón,
3 kwa maana upendo wako uko mbele yangu daima, nami natembea siku zote katika kweli yako.
Porque tu misericordia está delante de mis ojos Y ando en tu verdad.
4 Siketi pamoja na watu wadanganyifu, wala siandamani na wanafiki,
No me siento con hombres falsos Ni ando con hipócritas.
5 ninachukia kusanyiko la watenda mabaya na ninakataa kuketi pamoja na waovu.
Aborrezco la reunión de perversos Y no me sentaré con los inicuos.
6 Ninanawa mikono yangu kwa kuwa sina hatia, naikaribia madhabahu yako, Ee Bwana,
Lavaré en inocencia mis manos, Y así andaré en torno a tu altar, oh Yavé,
7 nikitangaza sifa yako kwa sauti kubwa, huku nikisimulia matendo yako ya ajabu.
Para hacer resonar mi voz de gratitud Y contar todas tus maravillas.
8 Ee Bwana, naipenda nyumba yako mahali unakoishi, mahali ambapo utukufu wako hukaa.
Oh Yavé, yo amo la Casa donde moras, Y el lugar donde reside tu gloria.
9 Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda dhambi, wala uhai wangu pamoja na wamwagao damu,
No arrebates mi alma con los pecadores, Ni mi vida con hombres sanguinarios,
10 ambao mikononi mwao kuna mipango miovu, ambao mikono yao ya kuume imejaa rushwa.
En las manos de los cuales está el crimen, Cuya mano derecha está llena de sobornos.
11 Bali mimi ninaishi maisha yasiyo na lawama; nikomboe na unihurumie.
En cuanto a mí, andaré en mi integridad. ¡Redímeme y ten misericordia de mí!
12 Miguu yangu imesimama katika uwanja tambarare; katika kusanyiko kuu nitamsifu Bwana.
Mis pies están en suelo firme. Bendeciré a Yavé en las congregaciones.

< Zaburi 26 >