< Zaburi 26 >
1 Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, nithibitishe katika haki, maana nimeishi maisha yasiyo na lawama; nimemtumainia Bwana bila kusitasita.
Un Salmo de David. Confirma que soy inocente, Señor, porque he actuado con integridad, y he confiado en el Señor sin falta.
2 Ee Bwana, unijaribu, unipime, uuchunguze moyo wangu na mawazo yangu;
Examíname, Señor, pruébame; investiga mi corazón y mi mente.
3 kwa maana upendo wako uko mbele yangu daima, nami natembea siku zote katika kweli yako.
Porque yo siempre recuerdo tu amor fiel, y sigo tu verdad.
4 Siketi pamoja na watu wadanganyifu, wala siandamani na wanafiki,
No me junto con mentirosos, ni me asocio con hipócritas.
5 ninachukia kusanyiko la watenda mabaya na ninakataa kuketi pamoja na waovu.
Me rehúso a estar junto a aquellos que hacen el mal, y no me veré envuelto con los malvados.
6 Ninanawa mikono yangu kwa kuwa sina hatia, naikaribia madhabahu yako, Ee Bwana,
Lavo mis manos para mostrar mi inocencia. Vengo a adorar a tu altar, Señor,
7 nikitangaza sifa yako kwa sauti kubwa, huku nikisimulia matendo yako ya ajabu.
cantando mis agradecimientos, contando todas las cosas maravillosas cosas que has hecho.
8 Ee Bwana, naipenda nyumba yako mahali unakoishi, mahali ambapo utukufu wako hukaa.
Señor, amo tu casa, el lugar donde vives en tu gloria.
9 Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda dhambi, wala uhai wangu pamoja na wamwagao damu,
Por favor, no me lances lejos con los pecadores. No me incluyas con aquellos que cometieron asesinatos,
10 ambao mikononi mwao kuna mipango miovu, ambao mikono yao ya kuume imejaa rushwa.
y cuyas manos cargan sus planes malvados y sobornos.
11 Bali mimi ninaishi maisha yasiyo na lawama; nikomboe na unihurumie.
Porque yo no hago eso, yo actúo con integridad. ¡Sálvame, y ten gracia conmigo!
12 Miguu yangu imesimama katika uwanja tambarare; katika kusanyiko kuu nitamsifu Bwana.
Estoy a favor de lo que es correcto, y alabaré al Señor cuando nos reunamos a adorarle.