< Zaburi 26 >

1 Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, nithibitishe katika haki, maana nimeishi maisha yasiyo na lawama; nimemtumainia Bwana bila kusitasita.
De David. Hazme justicia, oh Yahvé: he procedido con integridad: y, puesta en Yahvé mi confianza, no he vacilado.
2 Ee Bwana, unijaribu, unipime, uuchunguze moyo wangu na mawazo yangu;
Escrútame, Yahvé, y sondéame; acrisola mi conciencia y mi corazón.
3 kwa maana upendo wako uko mbele yangu daima, nami natembea siku zote katika kweli yako.
Porque, teniendo tu bondad presente a mis ojos, anduve según tu verdad.
4 Siketi pamoja na watu wadanganyifu, wala siandamani na wanafiki,
No he tomado asiento con hombres inicuos, ni busqué la compañía de los que fingen;
5 ninachukia kusanyiko la watenda mabaya na ninakataa kuketi pamoja na waovu.
aborrecí la sociedad de los malvados, y con los impíos no tuve comunicación.
6 Ninanawa mikono yangu kwa kuwa sina hatia, naikaribia madhabahu yako, Ee Bwana,
Lavo mis manos como inocente y rodeo tu altar, oh Yahvé,
7 nikitangaza sifa yako kwa sauti kubwa, huku nikisimulia matendo yako ya ajabu.
para levantar mi voz en tu alabanza y narrar todas tus maravillas.
8 Ee Bwana, naipenda nyumba yako mahali unakoishi, mahali ambapo utukufu wako hukaa.
Amo, Yahvé, la casa de tu morada, el lugar del tabernáculo de tu gloria.
9 Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda dhambi, wala uhai wangu pamoja na wamwagao damu,
No quieras juntar mi alma con los pecadores, ni mi vida con los sanguinarios,
10 ambao mikononi mwao kuna mipango miovu, ambao mikono yao ya kuume imejaa rushwa.
que en sus manos tienen crimen, y cuya diestra está llena de soborno,
11 Bali mimi ninaishi maisha yasiyo na lawama; nikomboe na unihurumie.
en tanto que yo he procedido con integridad; sálvame y apiádate de mí.
12 Miguu yangu imesimama katika uwanja tambarare; katika kusanyiko kuu nitamsifu Bwana.
Ya está mi pie sobre camino llano; en las asambleas bendeciré a Yahvé.

< Zaburi 26 >