< Zaburi 26 >

1 Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, nithibitishe katika haki, maana nimeishi maisha yasiyo na lawama; nimemtumainia Bwana bila kusitasita.
Суди ми, Господи, яко аз незлобою моею ходих: и на Господа уповая не изнемогу.
2 Ee Bwana, unijaribu, unipime, uuchunguze moyo wangu na mawazo yangu;
Искуси мя, Господи, и испытай мя, разжжи утробы моя и сердце мое.
3 kwa maana upendo wako uko mbele yangu daima, nami natembea siku zote katika kweli yako.
Яко милость Твоя пред очима моима есть, и благоугодих во истине Твоей.
4 Siketi pamoja na watu wadanganyifu, wala siandamani na wanafiki,
Не седох с сонмом суетным, и со законопреступными не вниду.
5 ninachukia kusanyiko la watenda mabaya na ninakataa kuketi pamoja na waovu.
Возненавидех церковь лукавнующих, и с нечестивыми не сяду.
6 Ninanawa mikono yangu kwa kuwa sina hatia, naikaribia madhabahu yako, Ee Bwana,
Умыю в неповинных руце мои, и обыду жертвенник Твой, Господи,
7 nikitangaza sifa yako kwa sauti kubwa, huku nikisimulia matendo yako ya ajabu.
еже услышати ми глас хвалы Твоея и поведати вся чудеса Твоя.
8 Ee Bwana, naipenda nyumba yako mahali unakoishi, mahali ambapo utukufu wako hukaa.
Господи, возлюбих благолепие дому Твоего и место селения славы Твоея.
9 Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda dhambi, wala uhai wangu pamoja na wamwagao damu,
Да не погубиши с нечестивыми душу мою и с мужи кровей живот мой,
10 ambao mikononi mwao kuna mipango miovu, ambao mikono yao ya kuume imejaa rushwa.
ихже в руку беззакония, десница их исполнися мзды.
11 Bali mimi ninaishi maisha yasiyo na lawama; nikomboe na unihurumie.
Аз же незлобою моею ходих: избави мя, Господи, и помилуй мя.
12 Miguu yangu imesimama katika uwanja tambarare; katika kusanyiko kuu nitamsifu Bwana.
Нога моя ста на правоте: в церквах благословлю Тя, Господи.

< Zaburi 26 >