< Zaburi 26 >
1 Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, nithibitishe katika haki, maana nimeishi maisha yasiyo na lawama; nimemtumainia Bwana bila kusitasita.
Julga-me, Senhor, pois tenho andado em minha sinceridade; tenho confiado tambem no Senhor; não vacillarei.
2 Ee Bwana, unijaribu, unipime, uuchunguze moyo wangu na mawazo yangu;
Examina-me, Senhor, e prova-me: esquadrinha os meus rins e o meu coração.
3 kwa maana upendo wako uko mbele yangu daima, nami natembea siku zote katika kweli yako.
Porque a tua benignidade está diante dos meus olhos; e tenho andado na tua verdade.
4 Siketi pamoja na watu wadanganyifu, wala siandamani na wanafiki,
Não me tenho assentado com homens vãos, nem converso com os homens dissimulados.
5 ninachukia kusanyiko la watenda mabaya na ninakataa kuketi pamoja na waovu.
Tenho aborrecido a congregação de malfeitores; nem me ajunto com os impios.
6 Ninanawa mikono yangu kwa kuwa sina hatia, naikaribia madhabahu yako, Ee Bwana,
Lavo as minhas mãos na innocencia; e assim andarei, Senhor, ao redor do teu altar.
7 nikitangaza sifa yako kwa sauti kubwa, huku nikisimulia matendo yako ya ajabu.
Para publicar com voz de louvor, e contar todas as tuas maravilhas.
8 Ee Bwana, naipenda nyumba yako mahali unakoishi, mahali ambapo utukufu wako hukaa.
Senhor, eu tenho amado a habitação da tua casa e o logar onde permanece a tua gloria.
9 Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda dhambi, wala uhai wangu pamoja na wamwagao damu,
Não apanhes a minha alma com os peccadores, nem a minha vida com os homens sanguinolentos,
10 ambao mikononi mwao kuna mipango miovu, ambao mikono yao ya kuume imejaa rushwa.
Em cujas mãos ha maleficio, e cuja mão direita está cheia de subornos.
11 Bali mimi ninaishi maisha yasiyo na lawama; nikomboe na unihurumie.
Mas eu ando na minha sinceridade; livra-me e tem piedade de mim.
12 Miguu yangu imesimama katika uwanja tambarare; katika kusanyiko kuu nitamsifu Bwana.
O meu pé está posto em caminho plano; nas congregações louvarei ao Senhor.