< Zaburi 26 >

1 Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, nithibitishe katika haki, maana nimeishi maisha yasiyo na lawama; nimemtumainia Bwana bila kusitasita.
مزمور داوود. ای خداوند، به داد من برس، زیرا در کمال صداقت رفتار می‌کنم و توکل راسخ به تو دارم.
2 Ee Bwana, unijaribu, unipime, uuchunguze moyo wangu na mawazo yangu;
خداوندا، مرا بیازما. فکر و دل مرا تفتیش کن و پاک ساز؛
3 kwa maana upendo wako uko mbele yangu daima, nami natembea siku zote katika kweli yako.
زیرا محبت تو را در نظر دارم و وفاداری تو را شعار زندگی خود کرده‌ام.
4 Siketi pamoja na watu wadanganyifu, wala siandamani na wanafiki,
با مردان نادرست همنشین نمی‌شوم و با اشخاص ریاکار رفت و آمد نمی‌کنم.
5 ninachukia kusanyiko la watenda mabaya na ninakataa kuketi pamoja na waovu.
از بدکاران نفرت دارم و با شریران معاشرت نمی‌کنم.
6 Ninanawa mikono yangu kwa kuwa sina hatia, naikaribia madhabahu yako, Ee Bwana,
دستهای خود را خواهم شست تا نشان دهم که بی‌گناهم، سپس مذبح تو را طواف خواهم کرد.
7 nikitangaza sifa yako kwa sauti kubwa, huku nikisimulia matendo yako ya ajabu.
آنگاه با سراییدن سرود شکرگزاری کارهای شگفت‌انگیز تو را به همه خبر خواهم داد.
8 Ee Bwana, naipenda nyumba yako mahali unakoishi, mahali ambapo utukufu wako hukaa.
خداوندا، خانهٔ تو را که حضور پرجلالت در آنجاست، دوست می‌دارم.
9 Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda dhambi, wala uhai wangu pamoja na wamwagao damu,
پس با من مانند بدکاران و قاتلان رفتار نکن که رشوه می‌دهند و خون مردم را می‌ریزند.
10 ambao mikononi mwao kuna mipango miovu, ambao mikono yao ya kuume imejaa rushwa.
11 Bali mimi ninaishi maisha yasiyo na lawama; nikomboe na unihurumie.
اما من راستی را پیشه کرده‌ام؛ بر من رحم کن و مرا نجات ده.
12 Miguu yangu imesimama katika uwanja tambarare; katika kusanyiko kuu nitamsifu Bwana.
خداوند را در حضور مردم سپاس خواهم گفت، زیرا مرا از خطر رهانیده است.

< Zaburi 26 >