< Zaburi 26 >
1 Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, nithibitishe katika haki, maana nimeishi maisha yasiyo na lawama; nimemtumainia Bwana bila kusitasita.
Von David. Richte du mich, o HERR; denn ich bin in meiner Unschuld gewandelt und habe mein Vertrauen auf den HERRN gesetzt; ich werde nicht wanken.
2 Ee Bwana, unijaribu, unipime, uuchunguze moyo wangu na mawazo yangu;
Prüfe mich, HERR, und erprobe mich; läutere meine Nieren und mein Herz!
3 kwa maana upendo wako uko mbele yangu daima, nami natembea siku zote katika kweli yako.
Denn deine Gnade war mir vor Augen, und ich wandelte in deiner Wahrheit.
4 Siketi pamoja na watu wadanganyifu, wala siandamani na wanafiki,
Ich blieb nie bei falschen Leuten und gehe nicht zu Hinterlistigen.
5 ninachukia kusanyiko la watenda mabaya na ninakataa kuketi pamoja na waovu.
Ich hasse die Versammlung der Boshaften und sitze nicht bei den Gottlosen.
6 Ninanawa mikono yangu kwa kuwa sina hatia, naikaribia madhabahu yako, Ee Bwana,
Ich wasche meine Hände in Unschuld und halte mich, HERR, zu deinem Altar,
7 nikitangaza sifa yako kwa sauti kubwa, huku nikisimulia matendo yako ya ajabu.
um Lobgesang erschallen zu lassen und alle deine Wunder zu erzählen.
8 Ee Bwana, naipenda nyumba yako mahali unakoishi, mahali ambapo utukufu wako hukaa.
HERR, ich habe lieb die Stätte deines Hauses und den Ort, da deine Herrlichkeit wohnt!
9 Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda dhambi, wala uhai wangu pamoja na wamwagao damu,
Raffe meine Seele nicht hin mit den Sündern, noch mein Leben mit den Blutgierigen,
10 ambao mikononi mwao kuna mipango miovu, ambao mikono yao ya kuume imejaa rushwa.
an deren Händen Laster klebt und deren Rechte voll Bestechung ist.
11 Bali mimi ninaishi maisha yasiyo na lawama; nikomboe na unihurumie.
Ich aber wandle in meiner Unschuld; erlöse mich und sei mir gnädig!
12 Miguu yangu imesimama katika uwanja tambarare; katika kusanyiko kuu nitamsifu Bwana.
Mein Fuß steht auf ebenem Boden; ich will den HERRN loben in den Versammlungen.