< Zaburi 26 >

1 Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, nithibitishe katika haki, maana nimeishi maisha yasiyo na lawama; nimemtumainia Bwana bila kusitasita.
Von David. Schaffe mir Recht, o HERR,
2 Ee Bwana, unijaribu, unipime, uuchunguze moyo wangu na mawazo yangu;
Prüfe mich, HERR, und erprobe mich: meine Nieren und mein Herz sind geläutert!
3 kwa maana upendo wako uko mbele yangu daima, nami natembea siku zote katika kweli yako.
Denn deine Gnade steht mir vor Augen, und ich wandle in deiner Wahrheit.
4 Siketi pamoja na watu wadanganyifu, wala siandamani na wanafiki,
Ich sitze nicht bei falschen Menschen und verkehre nicht mit hinterlistigen Leuten;
5 ninachukia kusanyiko la watenda mabaya na ninakataa kuketi pamoja na waovu.
ich meide die Versammlung der Missetäter und halte mich nicht zu den Gottlosen;
6 Ninanawa mikono yangu kwa kuwa sina hatia, naikaribia madhabahu yako, Ee Bwana,
ich wasche in Unschuld meine Hände und schreite so um deinen Altar, o HERR,
7 nikitangaza sifa yako kwa sauti kubwa, huku nikisimulia matendo yako ya ajabu.
daß ich laut ein Danklied erschallen lasse und alle deine Wundertaten verkünde.
8 Ee Bwana, naipenda nyumba yako mahali unakoishi, mahali ambapo utukufu wako hukaa.
O HERR, ich habe lieb die Stätte deines Hauses und den Ort, wo deine Herrlichkeit wohnt.
9 Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda dhambi, wala uhai wangu pamoja na wamwagao damu,
Raffe nicht weg meine Seele mit den (Seelen der) Sünder, noch mein Leben mit dem der Mordgesellen,
10 ambao mikononi mwao kuna mipango miovu, ambao mikono yao ya kuume imejaa rushwa.
an deren Händen Verbrechen kleben und deren Rechte gefüllt ist mit Bestechung!
11 Bali mimi ninaishi maisha yasiyo na lawama; nikomboe na unihurumie.
Ich aber wandle in meiner Unschuld: erlöse mich, HERR, und sei mir gnädig!
12 Miguu yangu imesimama katika uwanja tambarare; katika kusanyiko kuu nitamsifu Bwana.
Mein Fuß steht fest auf ebenem Plan: in Versammlungen will ich preisen den HERRN.

< Zaburi 26 >