< Zaburi 26 >

1 Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, nithibitishe katika haki, maana nimeishi maisha yasiyo na lawama; nimemtumainia Bwana bila kusitasita.
Of David - vindicate me O Yahweh for I in integrity my I have walked and in Yahweh I have trusted not I will slip.
2 Ee Bwana, unijaribu, unipime, uuchunguze moyo wangu na mawazo yangu;
Test me O Yahweh and put to [the] test me (test! *Q(k)*) kidneys my and heart my.
3 kwa maana upendo wako uko mbele yangu daima, nami natembea siku zote katika kweli yako.
For covenant loyalty your [is] to before eyes my and I walk about in faithfulness your.
4 Siketi pamoja na watu wadanganyifu, wala siandamani na wanafiki,
Not I sit with men of falsehood and with [those who] conceal themselves not I go.
5 ninachukia kusanyiko la watenda mabaya na ninakataa kuketi pamoja na waovu.
I hate [the] assembly of evil-doers and with wicked [people] not I sit.
6 Ninanawa mikono yangu kwa kuwa sina hatia, naikaribia madhabahu yako, Ee Bwana,
I wash in innocence hands my and I go around altar your O Yahweh.
7 nikitangaza sifa yako kwa sauti kubwa, huku nikisimulia matendo yako ya ajabu.
To make heard a sound of thanksgiving and to recount all wonders your.
8 Ee Bwana, naipenda nyumba yako mahali unakoishi, mahali ambapo utukufu wako hukaa.
O Yahweh I love [the] habitation of house your and [the] place of [the] dwelling of glory your.
9 Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda dhambi, wala uhai wangu pamoja na wamwagao damu,
May not you remove with sinners life my and with people of blood life my.
10 ambao mikononi mwao kuna mipango miovu, ambao mikono yao ya kuume imejaa rushwa.
[those] whom [is] in Hands their wickedness and right [hand] their it is full a bribe.
11 Bali mimi ninaishi maisha yasiyo na lawama; nikomboe na unihurumie.
And I in integrity my I will walk redeem me and show favor to me.
12 Miguu yangu imesimama katika uwanja tambarare; katika kusanyiko kuu nitamsifu Bwana.
Foot my it has stood on level ground in assemblies I will bless Yahweh.

< Zaburi 26 >