< Zaburi 26 >
1 Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, nithibitishe katika haki, maana nimeishi maisha yasiyo na lawama; nimemtumainia Bwana bila kusitasita.
Of David. Vindicate me, O LORD! For I have walked with integrity; I have trusted in the LORD without wavering.
2 Ee Bwana, unijaribu, unipime, uuchunguze moyo wangu na mawazo yangu;
Test me, O LORD, and try me; examine my heart and mind.
3 kwa maana upendo wako uko mbele yangu daima, nami natembea siku zote katika kweli yako.
For Your loving devotion is before my eyes, and I have walked in Your truth.
4 Siketi pamoja na watu wadanganyifu, wala siandamani na wanafiki,
I do not sit with deceitful men, nor keep company with hypocrites.
5 ninachukia kusanyiko la watenda mabaya na ninakataa kuketi pamoja na waovu.
I hate the mob of evildoers, and refuse to sit with the wicked.
6 Ninanawa mikono yangu kwa kuwa sina hatia, naikaribia madhabahu yako, Ee Bwana,
I wash my hands in innocence that I may go about Your altar, O LORD,
7 nikitangaza sifa yako kwa sauti kubwa, huku nikisimulia matendo yako ya ajabu.
to raise my voice in thanksgiving and declare all Your wonderful works.
8 Ee Bwana, naipenda nyumba yako mahali unakoishi, mahali ambapo utukufu wako hukaa.
O LORD, I love the house where You dwell, the place where Your glory resides.
9 Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda dhambi, wala uhai wangu pamoja na wamwagao damu,
Do not take my soul away with sinners, or my life with men of bloodshed,
10 ambao mikononi mwao kuna mipango miovu, ambao mikono yao ya kuume imejaa rushwa.
in whose hands are wicked schemes, whose right hands are full of bribes.
11 Bali mimi ninaishi maisha yasiyo na lawama; nikomboe na unihurumie.
But I will walk with integrity; redeem me and be merciful to me.
12 Miguu yangu imesimama katika uwanja tambarare; katika kusanyiko kuu nitamsifu Bwana.
My feet stand on level ground; in the congregations I will bless the LORD.