< Zaburi 25 >
1 Zaburi ya Daudi. Kwako wewe, Ee Bwana, nainua nafsi yangu,
ダビデの歌 主よ、わが魂はあなたを仰ぎ望みます。
2 ni wewe ninayekutumainia, Ee Mungu wangu. Usiniache niaibike, wala usiache adui zangu wakanishinda.
わが神よ、わたしはあなたに信頼します。どうか、わたしをはずかしめず、わたしの敵を勝ち誇らせないでください。
3 Kamwe hakuna hata mmoja anayekutegemea atakayeaibishwa, bali wataaibishwa wafanyao hila bila sababu.
すべてあなたを待ち望む者をはずかしめず、みだりに信義にそむく者をはずかしめてください。
4 Nionyeshe njia zako, Ee Bwana, nifundishe mapito yako,
主よ、あなたの大路をわたしに知らせ、あなたの道をわたしに教えてください。
5 niongoze katika kweli yako na kunifundisha, kwa maana wewe ni Mungu Mwokozi wangu, nalo tumaini langu liko kwako wakati wote.
あなたのまことをもって、わたしを導き、わたしを教えてください。あなたはわが救の神です。わたしはひねもすあなたを待ち望みます。
6 Kumbuka, Ee Bwana, rehema zako kuu na upendo, kwa maana zimekuwepo tangu zamani.
主よ、あなたのあわれみと、いつくしみとを思い出してください。これはいにしえから絶えることがなかったのです。
7 Usizikumbuke dhambi za ujana wangu wala njia zangu za uasi, sawasawa na upendo wako unikumbuke, kwa maana wewe ni mwema, Ee Bwana.
わたしの若き時の罪と、とがとを思い出さないでください。主よ、あなたの恵みのゆえに、あなたのいつくしみにしたがって、わたしを思い出してください。
8 Bwana ni mwema na mwenye adili, kwa hiyo huwafundisha wenye dhambi njia zake.
主は恵みふかく、かつ正しくいらせられる。それゆえ、主は道を罪びとに教え、
9 Huwaongoza wanyenyekevu katika haki, naye huwafundisha njia yake.
へりくだる者を公義に導き、へりくだる者にその道を教えられる。
10 Njia zote za Bwana ni za upendo na uaminifu kwa wale wanaoshika shuhuda za agano lake.
主のすべての道はその契約とあかしとを守る者にはいつくしみであり、まことである。
11 Ee Bwana, kwa ajili ya jina lako, unisamehe uovu wangu, ijapokuwa ni mwingi.
主よ、み名のために、わたしの罪をおゆるしください。わたしの罪は大きいのです。
12 Ni nani basi, mtu yule anayemcha Bwana? Atamfundisha katika njia atakayoichagua kwa ajili yake.
主を恐れる人はだれか。主はその選ぶべき道をその人に教えられる。
13 Mtu huyo atafanikiwa maishani mwake, nao wazao wake watairithi nchi.
彼はみずからさいわいに住まい、そのすえは地を継ぐであろう。
14 Siri ya Bwana iko kwa wale wamchao, yeye huwajulisha agano lake.
主の親しみは主をおそれる者のためにあり、主はその契約を彼らに知らせられる。
15 Macho yangu humwelekea Bwana daima, kwa kuwa yeye peke yake ndiye ataitoa miguu yangu kutoka mtego.
わたしの目は常に主に向かっている。主はわたしの足を網から取り出されるからである。
16 Nigeukie na unihurumie, kwa maana mimi ni mpweke na mwenye kuteseka.
わたしをかえりみ、わたしをあわれんでください。わたしはひとりわびしく苦しんでいるのです。
17 Shida za moyo wangu zimeongezeka, niokoe katika dhiki yangu.
わたしの心の悩みをゆるめ、わたしを苦しみから引き出してください。
18 Uangalie mateso na shida zangu na uniondolee dhambi zangu zote.
わたしの苦しみ悩みをかえりみ、わたしのすべての罪をおゆるしください。
19 Tazama adui zangu walivyo wengi, pia uone jinsi wanavyonichukia vikali!
わたしの敵がいかに多く、かつ激しい憎しみをもってわたしを憎んでいるかをごらんください。
20 Uyalinde maisha yangu na uniokoe, usiniache niaibike, kwa maana nimekukimbilia wewe.
わたしの魂を守り、わたしをお助けください。わたしをはずかしめないでください。わたしはあなたに寄り頼んでいます。
21 Uadilifu na uaminifu vinilinde, kwa sababu tumaini langu ni kwako.
どうか、誠実と潔白とが、わたしを守ってくれるように。わたしはあなたを待ち望んでいます。
22 Ee Mungu, wakomboe Israeli, katika shida zao zote!
神よ、イスラエルをあがない、すべての悩みから救いだしてください。