< Zaburi 25 >

1 Zaburi ya Daudi. Kwako wewe, Ee Bwana, nainua nafsi yangu,
Van David. Tot U verhef ik mijn ziel, O Jahweh, mijn God!
2 ni wewe ninayekutumainia, Ee Mungu wangu. Usiniache niaibike, wala usiache adui zangu wakanishinda.
Op U blijf ik hopen; laat mij niet worden beschaamd, En den vijand niet de spot met mij drijven.
3 Kamwe hakuna hata mmoja anayekutegemea atakayeaibishwa, bali wataaibishwa wafanyao hila bila sababu.
Neen, niemand die op U vertrouwt, wordt beschaamd; Alleen de afvalligen worden te schande.
4 Nionyeshe njia zako, Ee Bwana, nifundishe mapito yako,
Jahweh, toon mij uw wegen, En maak mij uw paden bekend;
5 niongoze katika kweli yako na kunifundisha, kwa maana wewe ni Mungu Mwokozi wangu, nalo tumaini langu liko kwako wakati wote.
Laat mij wandelen in uw waarheid, Onderricht mij, want Gij zijt de God van mijn heil. Op U blijf ik altijd vertrouwen, Om uw goedheid, o Jahweh!
6 Kumbuka, Ee Bwana, rehema zako kuu na upendo, kwa maana zimekuwepo tangu zamani.
Gedenk uw barmhartigheid, Jahweh; En uw ontferming, want ze zijn eeuwig!
7 Usizikumbuke dhambi za ujana wangu wala njia zangu za uasi, sawasawa na upendo wako unikumbuke, kwa maana wewe ni mwema, Ee Bwana.
Wees niet de zonden mijner jeugd en mijn fouten indachtig, Maar blijf mij gedenken naar uw genade.
8 Bwana ni mwema na mwenye adili, kwa hiyo huwafundisha wenye dhambi njia zake.
Jahweh is goed en minzaam: Daarom wijst Hij de zondaars terecht.
9 Huwaongoza wanyenyekevu katika haki, naye huwafundisha njia yake.
De nederigen houdt Hij in het rechte spoor, Den eenvoudige toont Hij zijn pad;
10 Njia zote za Bwana ni za upendo na uaminifu kwa wale wanaoshika shuhuda za agano lake.
Alle wegen van Jahweh zijn goedheid en trouw, Voor wie zijn Verbond en zijn Wet onderhoudt.
11 Ee Bwana, kwa ajili ya jina lako, unisamehe uovu wangu, ijapokuwa ni mwingi.
O Jahweh, om wille van uw Naam, Vergeef mij mijn schuld, hoe groot zij ook is.
12 Ni nani basi, mtu yule anayemcha Bwana? Atamfundisha katika njia atakayoichagua kwa ajili yake.
Iedereen, die Jahweh vreest, Leert Hij, welke weg hij moet kiezen:
13 Mtu huyo atafanikiwa maishani mwake, nao wazao wake watairithi nchi.
Hijzelf zal steeds in voorspoed leven, Zijn kinderen zullen het Land bezitten.
14 Siri ya Bwana iko kwa wale wamchao, yeye huwajulisha agano lake.
Jahweh’s vriendschap geldt hun, die Hem vrezen, Hij maakt hen deelachtig aan zijn Verbond.
15 Macho yangu humwelekea Bwana daima, kwa kuwa yeye peke yake ndiye ataitoa miguu yangu kutoka mtego.
Mijn ogen zijn altijd op Jahweh gericht; Want Hij trekt mijn voet uit de strikken.
16 Nigeukie na unihurumie, kwa maana mimi ni mpweke na mwenye kuteseka.
Wend U tot mij, en wees mij genadig, Want ik ben eenzaam, ellendig.
17 Shida za moyo wangu zimeongezeka, niokoe katika dhiki yangu.
Verlicht de druk van mijn hart, En bevrijd me van mijn benauwdheid!
18 Uangalie mateso na shida zangu na uniondolee dhambi zangu zote.
Blik neer op mijn ellende en jammer, En vergeef mij al mijn zonden.
19 Tazama adui zangu walivyo wengi, pia uone jinsi wanavyonichukia vikali!
Zie, hoe talrijk mijn vijanden zijn, En hoe diep ze mij haten.
20 Uyalinde maisha yangu na uniokoe, usiniache niaibike, kwa maana nimekukimbilia wewe.
Behoed mij, en red mij; Laat mijn vertrouwen op U niet worden beschaamd!
21 Uadilifu na uaminifu vinilinde, kwa sababu tumaini langu ni kwako.
Maar mogen onschuld en deugd mij beschermen; Want op U blijf ik hopen, o Jahweh!
22 Ee Mungu, wakomboe Israeli, katika shida zao zote!
Verlos Israël uit al zijn ellenden, o God!

< Zaburi 25 >