< Zaburi 24 >
1 Zaburi ya Daudi. Dunia ni mali ya Bwana, na vyote vilivyomo ndani yake, ulimwengu, na wote waishio ndani yake,
Del Signore è la terra e quanto contiene, l'universo e i suoi abitanti. Di Davide. Salmo.
2 maana aliiwekea misingi yake baharini na kuifanya imara juu ya maji.
E' lui che l'ha fondata sui mari, e sui fiumi l'ha stabilita.
3 Nani awezaye kuupanda mlima wa Bwana? Ni nani awezaye kusimama patakatifu pake?
Chi salirà il monte del Signore, chi starà nel suo luogo santo?
4 Ni yule mwenye mikono safi na moyo mweupe, yule ambaye hakuinulia sanamu nafsi yake au kuapa kwa kitu cha uongo.
Chi ha mani innocenti e cuore puro, chi non pronunzia menzogna, chi non giura a danno del suo prossimo.
5 Huyo atapokea baraka kutoka kwa Bwana, na hukumu ya haki kutoka kwa Mungu Mwokozi wake.
Otterrà benedizione dal Signore, giustizia da Dio sua salvezza.
6 Hiki ndicho kizazi cha wale wamtafutao, wale wautafutao uso wako, Ee Mungu wa Yakobo.
Ecco la generazione che lo cerca, che cerca il tuo volto, Dio di Giacobbe.
7 Inueni vichwa vyenu, enyi malango, inukeni enyi milango ya kale, ili mfalme wa utukufu apate kuingia.
Sollevate, porte, i vostri frontali, alzatevi, porte antiche, ed entri il re della gloria.
8 Ni nani huyu Mfalme wa utukufu? Ni Bwana aliye na nguvu na uweza, ni Bwana aliye hodari katika vita.
Chi è questo re della gloria? Il Signore forte e potente, il Signore potente in battaglia.
9 Inueni vichwa vyenu, enyi malango, viinueni juu enyi milango ya kale, ili Mfalme wa utukufu apate kuingia.
Sollevate, porte, i vostri frontali, alzatevi, porte antiche, ed entri il re della gloria.
10 Ni nani yeye, huyu Mfalme wa utukufu? Ni Bwana Mwenye Nguvu Zote; yeye ndiye Mfalme wa utukufu.
Chi è questo re della gloria? Il Signore degli eserciti è il re della gloria.