< Zaburi 24 >
1 Zaburi ya Daudi. Dunia ni mali ya Bwana, na vyote vilivyomo ndani yake, ulimwengu, na wote waishio ndani yake,
大衛的詩。 地和其中所充滿的, 世界和住在其間的,都屬耶和華。
2 maana aliiwekea misingi yake baharini na kuifanya imara juu ya maji.
他把地建立在海上, 安定在大水之上。
3 Nani awezaye kuupanda mlima wa Bwana? Ni nani awezaye kusimama patakatifu pake?
誰能登耶和華的山? 誰能站在他的聖所?
4 Ni yule mwenye mikono safi na moyo mweupe, yule ambaye hakuinulia sanamu nafsi yake au kuapa kwa kitu cha uongo.
就是手潔心清,不向虛妄, 起誓不懷詭詐的人。
5 Huyo atapokea baraka kutoka kwa Bwana, na hukumu ya haki kutoka kwa Mungu Mwokozi wake.
他必蒙耶和華賜福, 又蒙救他的上帝使他成義。
6 Hiki ndicho kizazi cha wale wamtafutao, wale wautafutao uso wako, Ee Mungu wa Yakobo.
這是尋求耶和華的族類, 是尋求你面的雅各。 (細拉)
7 Inueni vichwa vyenu, enyi malango, inukeni enyi milango ya kale, ili mfalme wa utukufu apate kuingia.
眾城門哪,你們要抬起頭來! 永久的門戶,你們要被舉起! 那榮耀的王將要進來!
8 Ni nani huyu Mfalme wa utukufu? Ni Bwana aliye na nguvu na uweza, ni Bwana aliye hodari katika vita.
榮耀的王是誰呢? 就是有力有能的耶和華, 在戰場上有能的耶和華!
9 Inueni vichwa vyenu, enyi malango, viinueni juu enyi milango ya kale, ili Mfalme wa utukufu apate kuingia.
眾城門哪,你們要抬起頭來! 永久的門戶,你們要把頭抬起! 那榮耀的王將要進來!
10 Ni nani yeye, huyu Mfalme wa utukufu? Ni Bwana Mwenye Nguvu Zote; yeye ndiye Mfalme wa utukufu.
榮耀的王是誰呢? 萬軍之耶和華, 他是榮耀的王! (細拉)