< Zaburi 23 >
1 Zaburi ya Daudi. Bwana ndiye mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu.
Davut'un mezmuru RAB çobanımdır, Eksiğim olmaz.
2 Hunilaza katika malisho ya majani mabichi, kando ya maji matulivu huniongoza,
Beni yemyeşil çayırlarda yatırır, Sakin suların kıyısına götürür.
3 hunihuisha nafsi yangu. Huniongoza katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.
İçimi tazeler, Adı uğruna bana doğru yollarda öncülük eder.
4 Hata kama nikipita katikati ya bonde la uvuli wa mauti, sitaogopa mabaya, kwa maana wewe upo pamoja nami; fimbo yako na mkongojo wako vyanifariji.
Karanlık ölüm vadisinden geçsem bile, Kötülükten korkmam. Çünkü sen benimlesin. Çomağın, değneğin güven verir bana.
5 Waandaa meza mbele yangu machoni pa adui zangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, kikombe changu kinafurika.
Düşmanlarımın önünde bana sofra kurarsın, Başıma yağ sürersin, Kâsem taşıyor.
6 Hakika wema na upendo vitanifuata siku zote za maisha yangu, nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele.
Ömrüm boyunca yalnız iyilik ve sevgi izleyecek beni, Hep RAB'bin evinde oturacağım.