< Zaburi 23 >

1 Zaburi ya Daudi. Bwana ndiye mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu.
Psalmo de David. La Eternulo estas mia paŝtisto; mi mankon ne havos.
2 Hunilaza katika malisho ya majani mabichi, kando ya maji matulivu huniongoza,
Sur verdaj herbejoj Li ripozigas min, Apud trankvilaj akvoj Li kondukas min.
3 hunihuisha nafsi yangu. Huniongoza katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.
Li kvietigas mian animon; Li kondukas min laŭ vojo de la vero, pro Sia nomo.
4 Hata kama nikipita katikati ya bonde la uvuli wa mauti, sitaogopa mabaya, kwa maana wewe upo pamoja nami; fimbo yako na mkongojo wako vyanifariji.
Eĉ kiam mi iros tra valo de densa mallumo, Mi ne timos malbonon, ĉar Vi estas kun mi; Via bastono kaj apogiĝilo trankviligos min.
5 Waandaa meza mbele yangu machoni pa adui zangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, kikombe changu kinafurika.
Vi kovras por mi tablon antaŭ miaj malamikoj; Vi ŝmiris per oleo mian kapon, mia pokalo estas plenigita.
6 Hakika wema na upendo vitanifuata siku zote za maisha yangu, nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele.
Nur bono kaj favoro sekvos min en la daŭro de mia tuta vivo; Kaj mi restos en la domo de la Eternulo eterne.

< Zaburi 23 >