< Zaburi 23 >
1 Zaburi ya Daudi. Bwana ndiye mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu.
大衛的詩。 耶和華是我的牧者, 我必不致缺乏。
2 Hunilaza katika malisho ya majani mabichi, kando ya maji matulivu huniongoza,
他使我躺臥在青草地上, 領我在可安歇的水邊。
3 hunihuisha nafsi yangu. Huniongoza katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.
他使我的靈魂甦醒, 為自己的名引導我走義路。
4 Hata kama nikipita katikati ya bonde la uvuli wa mauti, sitaogopa mabaya, kwa maana wewe upo pamoja nami; fimbo yako na mkongojo wako vyanifariji.
我雖然行過死蔭的幽谷, 也不怕遭害, 因為你與我同在; 你的杖,你的竿,都安慰我。
5 Waandaa meza mbele yangu machoni pa adui zangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, kikombe changu kinafurika.
在我敵人面前,你為我擺設筵席; 你用油膏了我的頭,使我的福杯滿溢。
6 Hakika wema na upendo vitanifuata siku zote za maisha yangu, nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele.
我一生一世必有恩惠慈愛隨着我; 我且要住在耶和華的殿中,直到永遠。