< Zaburi 22 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Kulungu wa Alfajiri.” Zaburi ya Daudi. Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa? Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu?
Al maestro de coro. Por el pronto socorro. Salmo de David. Dios mío, Dios mío, ¿por qué me has abandonado? Los gritos de mis pecados alejan de mí el socorro.
2 Ee Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu, hata usiku, sinyamazi.
Dios mío, clamo de día, y no respondes; de noche también, y no te cuidas de mí.
3 Hata hivyo umesimikwa katika kiti cha enzi kama Uliye Mtakatifu; wewe ni sifa ya Israeli.
Y Tú, sin embargo, estás en tu santa morada, ¡oh gloria de Israel!
4 Kwako wewe baba zetu waliweka tumaini lao, walikutumaini nawe ukawaokoa.
En Ti esperaron nuestros padres; esperaron, y los libraste.
5 Walikulilia wewe na ukawaokoa, walikutegemea wewe nao hawakuaibika.
A Ti clamaron, y fueron salvados; en Ti confiaron, y no quedaron confundidos.
6 Mimi ni mnyoo wala si mwanadamu, wanaume wamenibeza, na watu wamenidharau.
Pero es que yo soy gusano, y no hombre, oprobio de los hombres y desecho de la plebe.
7 Wote wanionao hunidhihaki, hunivurumishia matusi, wakitikisa vichwa vyao:
Cuantos me ven se mofan de mí, tuercen los labios y menean la cabeza:
8 Husema, “Anamtegemea Bwana, basi Bwana na amwokoe. Amkomboe basi, kwa maana anapendezwa naye.”
“Confió en Yahvé: que Él lo salve; líbrelo, ya que en Él se complace.”
9 Hata hivyo ulinitoa tumboni, ukanifanya nikutegemee, hata nilipokuwa ninanyonya matiti ya mama yangu.
Sí, Tú eres mi sostén desde el seno materno, mi refugio desde los pechos de mi madre.
10 Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa, toka tumboni mwa mama yangu umekuwa Mungu wangu.
A Ti fui entregado desde mi nacimiento; desde el vientre de mi madre Tú eres mi Dios.
11 Usiwe mbali nami, kwa maana shida iko karibu na hakuna wa kunisaidia.
No estés lejos de mí, porque la tribulación está cerca, porque no hay quien socorra.
12 Mafahali wengi wamenizunguka, mafahali wa Bashani wenye nguvu wamenizingira.
Me veo rodeado de muchos toros; los fuertes de Basan me cercan;
13 Simba wangurumao wanaorarua mawindo yao hupanua vinywa vyao dhidi yangu.
abren contra mí sus bocas, cual león rapaz y rugiente.
14 Nimemiminwa kama maji, mifupa yangu yote imetoka katika viungo vyake. Moyo wangu umegeuka kuwa nta, umeyeyuka ndani yangu.
Soy como agua derramada, todos mis huesos se han descoyuntado; mi corazón, como cera, se diluye en mis entrañas.
15 Nguvu zangu zimekauka kama kigae, ulimi wangu umegandamana na kaakaa la kinywa changu, kwa sababu umenilaza katika mavumbi ya kifo.
Mi garganta se ha secado como una teja; mi lengua se pega a mi paladar, me has reducido al polvo de la muerte.
16 Mbwa wamenizunguka, kundi la watu waovu limenizingira, wametoboa mikono yangu na miguu yangu.
Porque me han rodeado muchos perros; una caterva de malvados me encierra; han perforado mis manos y mis pies;
17 Naweza kuhesabu mifupa yangu yote, watu wananikodolea macho na kunisimanga.
puedo contar todos mis huesos. Entretanto, ellos miran, y al verme se alegran.
18 Wanagawana nguo zangu wao kwa wao, na vazi langu wanalipigia kura.
Se reparten mis vestidos, y sobre mi túnica echan suertes.
19 Lakini wewe, Ee Bwana, usiwe mbali. Ee Nguvu yangu, uje haraka unisaidie.
Mas Tú, Yahvé, no estés lejos de mí; sostén mío, apresúrate a socorrerme.
20 Okoa maisha yangu na upanga, uhai wangu wa thamani kutoka nguvu za mbwa.
Libra mi alma de la espada, mi vida del poder del perro.
21 Niokoe kutoka kinywani mwa simba, niokoe kutoka pembe za mafahali mwitu.
Sálvame de la boca del león; de entre las astas de los bisontes escúchame.
22 Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu, katika kusanyiko nitakusifu wewe.
Anunciaré tu Nombre a mis hermanos, y proclamaré tu alabanza en medio de la asamblea.
23 Ninyi ambao mnamcha Bwana, msifuni! Ninyi nyote wazao wote wa Yakobo, mheshimuni yeye! Mcheni yeye, ninyi wazao wote wa Israeli!
Los que teméis a Yahvé alabadle, glorificadle, vosotros todos, linaje de Israel.
24 Kwa maana hakupuuza wala kudharau mateso ya aliyeonewa; hakumficha uso wake bali alisikiliza kilio chake ili amsaidie.
Pues no despreció ni desatendió la miseria del miserable; no escondió de él su rostro, y cuando imploró su auxilio, le escuchó.
25 Kwako wewe hutoka kiini cha sifa zangu katika kusanyiko kubwa, nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wakuchao wewe.
Para Ti será mi alabanza en la gran asamblea, cumpliré mis votos en presencia de los que te temen.
26 Maskini watakula na kushiba, wale wamtafutao Bwana watamsifu: mioyo yenu na iishi milele!
Los pobres comerán y se hartarán, alabarán a Yahvé los que le buscan. Sus corazones vivirán para siempre.
27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kumgeukia Bwana, nazo jamaa zote za mataifa watasujudu mbele zake,
Recordándolo, volverán a Yahvé todos los confines de la tierra; y todas las naciones de los gentiles se postrarán ante su faz.
28 kwa maana ufalme ni wa Bwana naye hutawala juu ya mataifa.
Porque de Yahvé es el reino, y Él mismo gobernará a las naciones.
29 Matajiri wote wa dunia watasherehekea na kuabudu. Wote waendao mavumbini watapiga magoti mbele yake, wote ambao hawawezi kudumisha uhai wao.
A Él solo adorarán todos los que duermen bajo la tierra; ante Él se encorvará todo el que desciende al polvo, y no tiene ya vida en sí.
30 Wazao wa baadaye watamtumikia yeye; vizazi vijavyo vitajulishwa habari za Bwana.
Mi descendencia le servirá a Él y hablará de Yahvé a la edad venidera.
31 Watatangaza haki yake kwa watu ambao hawajazaliwa bado, kwa maana yeye ametenda hili.
Anunciará su justicia a un pueblo que ha de nacer: “Estas cosas ha hecho Yahvé.”

< Zaburi 22 >