< Zaburi 22 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Kulungu wa Alfajiri.” Zaburi ya Daudi. Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa? Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu?
Dāvida dziesma. Dziedātāju vadonim pēc: „rīta blāzmas stirna“. Mans Dievs! Mans Dievs! Kāpēc Tu mani esi atstājis? Tu esi tālu no manas palīdzības, no manas kaukšanas vārdiem.
2 Ee Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu, hata usiku, sinyamazi.
Mans Dievs, es saucu dienā, bet Tu man neatbildi, un nakti es arī klusu neciešu.
3 Hata hivyo umesimikwa katika kiti cha enzi kama Uliye Mtakatifu; wewe ni sifa ya Israeli.
Bet Tu esi svēts, dzīvodams starp Israēla slavas dziesmām.
4 Kwako wewe baba zetu waliweka tumaini lao, walikutumaini nawe ukawaokoa.
Uz Tevi mūsu tēvi cerējuši, tie ir cerējuši, un Tu tos esi izglābis.
5 Walikulilia wewe na ukawaokoa, walikutegemea wewe nao hawakuaibika.
Uz Tevi tie saukuši un ir izpestīti, tie cerējuši uz Tevi un nav palikuši kaunā.
6 Mimi ni mnyoo wala si mwanadamu, wanaume wamenibeza, na watu wamenidharau.
Bet es esmu tārps un ne cilvēks, cilvēku apsmiekls un ļaužu nicināts.
7 Wote wanionao hunidhihaki, hunivurumishia matusi, wakitikisa vichwa vyao:
Visi, kas mani redz, mani apmēda, atplēš lūpas un krata galvu sacīdami:
8 Husema, “Anamtegemea Bwana, basi Bwana na amwokoe. Amkomboe basi, kwa maana anapendezwa naye.”
Viņš to Tam Kungam sūdzējis; lai Tas viņu izrauj un viņu izglābj, ja Tam pie viņa ir labs prāts.
9 Hata hivyo ulinitoa tumboni, ukanifanya nikutegemee, hata nilipokuwa ninanyonya matiti ya mama yangu.
Tomēr Tu tas esi, kas mani izvedis no mātes miesām; Tu man licis paļauties uz Tevi no mātes krūtīm.
10 Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa, toka tumboni mwa mama yangu umekuwa Mungu wangu.
Uz Tevi es esmu mests no mātes klēpja, no mātes miesām Tu esi mans Dievs.
11 Usiwe mbali nami, kwa maana shida iko karibu na hakuna wa kunisaidia.
Neesi tālu no manis, jo bailība ir tuvu, jo palīga nav.
12 Mafahali wengi wamenizunguka, mafahali wa Bashani wenye nguvu wamenizingira.
Lieli vērši mani apstājuši, trekni buļļi ap mani apmetušies.
13 Simba wangurumao wanaorarua mawindo yao hupanua vinywa vyao dhidi yangu.
Tie atplēš savu rīkli pret mani kā lauva, plezdams un rūkdams.
14 Nimemiminwa kama maji, mifupa yangu yote imetoka katika viungo vyake. Moyo wangu umegeuka kuwa nta, umeyeyuka ndani yangu.
Es esmu izgāzts kā ūdens, visi mani kauli ir izlauzti, mana sirds ir manās miesās kā izkausēts vasks.
15 Nguvu zangu zimekauka kama kigae, ulimi wangu umegandamana na kaakaa la kinywa changu, kwa sababu umenilaza katika mavumbi ya kifo.
Mans spēks ir izkaltis kā poda gabals, un mana mēle līp pie mana zoda, un Tu mani nolieci nāves pīšļos,
16 Mbwa wamenizunguka, kundi la watu waovu limenizingira, wametoboa mikono yangu na miguu yangu.
Jo suņi mani apstājuši, un ļaundarītāju bars ap mani ir apmeties, tie manas rokas un manas kājas ir izurbuši.
17 Naweza kuhesabu mifupa yangu yote, watu wananikodolea macho na kunisimanga.
Es visus savus kaulus varu skaitīt, bet viņi skatās un lūko uz mani ar prieku.
18 Wanagawana nguo zangu wao kwa wao, na vazi langu wanalipigia kura.
Tie dala manas drēbes savā starpā un met kauliņus par manu apģērbu.
19 Lakini wewe, Ee Bwana, usiwe mbali. Ee Nguvu yangu, uje haraka unisaidie.
Bet Tu, ak Kungs, neesi tālu, mans stiprums, steidzies man palīgā.
20 Okoa maisha yangu na upanga, uhai wangu wa thamani kutoka nguvu za mbwa.
Izglāb manu dvēseli no zobena, manu vientuli no suņu varas.
21 Niokoe kutoka kinywani mwa simba, niokoe kutoka pembe za mafahali mwitu.
Izpestī mani no lauvas rīkles un paklausi mani no vēršu ragiem.
22 Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu, katika kusanyiko nitakusifu wewe.
Es sludināšu Tavu vārdu saviem brāļiem, es Tevi slavēšu draudzes vidū.
23 Ninyi ambao mnamcha Bwana, msifuni! Ninyi nyote wazao wote wa Yakobo, mheshimuni yeye! Mcheni yeye, ninyi wazao wote wa Israeli!
Slavējiet To Kungu, jūs, kas Viņu bīstaties, viss Jēkaba dzimums lai Viņu godā, un bīstaties, viss Israēla dzimums.
24 Kwa maana hakupuuza wala kudharau mateso ya aliyeonewa; hakumficha uso wake bali alisikiliza kilio chake ili amsaidie.
Jo Viņš nav nicinājis nedz apsmējis bēdīga bēdas, nedz no tā apslēpis Savu vaigu, un kad tas Viņu piesauca, tad Viņš paklausīja.
25 Kwako wewe hutoka kiini cha sifa zangu katika kusanyiko kubwa, nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wakuchao wewe.
No Tevis es dziedāšu tai lielā draudzē, es maksāšu savus solījumus to priekšā, kas Viņu bīstas.
26 Maskini watakula na kushiba, wale wamtafutao Bwana watamsifu: mioyo yenu na iishi milele!
Tie bēdīgie ēdīs un būs paēduši, un kas To Kungu meklē, Viņu slavēs; jūsu sirds dzīvos mūžīgi.
27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kumgeukia Bwana, nazo jamaa zote za mataifa watasujudu mbele zake,
Visi zemes gali to pieminēs un atgriezīsies pie Tā Kunga, un visas pagānu tautas klanīsies Viņa priekšā.
28 kwa maana ufalme ni wa Bwana naye hutawala juu ya mataifa.
Jo Tam Kungam pieder tā valstība, un Viņš valda pār tām tautām.
29 Matajiri wote wa dunia watasherehekea na kuabudu. Wote waendao mavumbini watapiga magoti mbele yake, wote ambao hawawezi kudumisha uhai wao.
Visi treknie virs zemes ēdīs un pielūgs, visi, kas pīšļos guļ, klanīsies Viņa priekšā, arī tie, kas nevarēja uzturēt savu dzīvību.
30 Wazao wa baadaye watamtumikia yeye; vizazi vijavyo vitajulishwa habari za Bwana.
Viņam būs dzimums, kas Viņam kalpos, par To Kungu sludinās līdz radu radiem;
31 Watatangaza haki yake kwa watu ambao hawajazaliwa bado, kwa maana yeye ametenda hili.
Nāks un sludinās Viņa taisnību tiem ļaudīm, kas vēl dzims, ka Viņš to ir darījis.

< Zaburi 22 >