< Zaburi 22 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Kulungu wa Alfajiri.” Zaburi ya Daudi. Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa? Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu?
in finem pro adsumptione matutina psalmus David Deus Deus meus respice me quare me dereliquisti longe a salute mea verba delictorum meorum
2 Ee Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu, hata usiku, sinyamazi.
Deus meus clamabo per diem et non exaudies et nocte et non ad insipientiam mihi
3 Hata hivyo umesimikwa katika kiti cha enzi kama Uliye Mtakatifu; wewe ni sifa ya Israeli.
tu autem in sancto habitas Laus Israhel
4 Kwako wewe baba zetu waliweka tumaini lao, walikutumaini nawe ukawaokoa.
in te speraverunt patres nostri speraverunt et liberasti eos
5 Walikulilia wewe na ukawaokoa, walikutegemea wewe nao hawakuaibika.
ad te clamaverunt et salvi facti sunt in te speraverunt et non sunt confusi
6 Mimi ni mnyoo wala si mwanadamu, wanaume wamenibeza, na watu wamenidharau.
ego autem sum vermis et non homo obprobrium hominum et abiectio plebis
7 Wote wanionao hunidhihaki, hunivurumishia matusi, wakitikisa vichwa vyao:
omnes videntes me deriserunt me locuti sunt labiis moverunt caput
8 Husema, “Anamtegemea Bwana, basi Bwana na amwokoe. Amkomboe basi, kwa maana anapendezwa naye.”
speravit in Domino eripiat eum salvum faciat eum quoniam vult eum
9 Hata hivyo ulinitoa tumboni, ukanifanya nikutegemee, hata nilipokuwa ninanyonya matiti ya mama yangu.
quoniam tu es qui extraxisti me de ventre spes mea ab uberibus matris meae
10 Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa, toka tumboni mwa mama yangu umekuwa Mungu wangu.
in te proiectus sum ex utero de ventre matris meae Deus meus es tu
11 Usiwe mbali nami, kwa maana shida iko karibu na hakuna wa kunisaidia.
ne discesseris a me quoniam tribulatio proxima est quoniam non est qui adiuvet
12 Mafahali wengi wamenizunguka, mafahali wa Bashani wenye nguvu wamenizingira.
circumdederunt me vituli multi tauri pingues obsederunt me
13 Simba wangurumao wanaorarua mawindo yao hupanua vinywa vyao dhidi yangu.
aperuerunt super me os suum sicut leo rapiens et rugiens
14 Nimemiminwa kama maji, mifupa yangu yote imetoka katika viungo vyake. Moyo wangu umegeuka kuwa nta, umeyeyuka ndani yangu.
sicut aqua effusus sum et dispersa sunt universa ossa mea factum est cor meum tamquam cera liquescens in medio ventris mei
15 Nguvu zangu zimekauka kama kigae, ulimi wangu umegandamana na kaakaa la kinywa changu, kwa sababu umenilaza katika mavumbi ya kifo.
aruit tamquam testa virtus mea et lingua mea adhesit faucibus meis et in limum mortis deduxisti me
16 Mbwa wamenizunguka, kundi la watu waovu limenizingira, wametoboa mikono yangu na miguu yangu.
quoniam circumdederunt me canes multi concilium malignantium obsedit me foderunt manus meas et pedes meos
17 Naweza kuhesabu mifupa yangu yote, watu wananikodolea macho na kunisimanga.
dinumeraverunt omnia ossa mea ipsi vero consideraverunt et inspexerunt me
18 Wanagawana nguo zangu wao kwa wao, na vazi langu wanalipigia kura.
diviserunt sibi vestimenta mea et super vestem meam miserunt sortem
19 Lakini wewe, Ee Bwana, usiwe mbali. Ee Nguvu yangu, uje haraka unisaidie.
tu autem Domine ne elongaveris auxilium tuum ad defensionem meam conspice
20 Okoa maisha yangu na upanga, uhai wangu wa thamani kutoka nguvu za mbwa.
erue a framea animam meam et de manu canis unicam meam
21 Niokoe kutoka kinywani mwa simba, niokoe kutoka pembe za mafahali mwitu.
salva me ex ore leonis et a cornibus unicornium humilitatem meam
22 Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu, katika kusanyiko nitakusifu wewe.
narrabo nomen tuum fratribus meis in media ecclesia laudabo te
23 Ninyi ambao mnamcha Bwana, msifuni! Ninyi nyote wazao wote wa Yakobo, mheshimuni yeye! Mcheni yeye, ninyi wazao wote wa Israeli!
qui timetis Dominum laudate eum universum semen Iacob magnificate eum
24 Kwa maana hakupuuza wala kudharau mateso ya aliyeonewa; hakumficha uso wake bali alisikiliza kilio chake ili amsaidie.
timeat eum omne semen Israhel quoniam non sprevit neque dispexit deprecationem pauperis nec avertit faciem suam a me et cum clamarem ad eum exaudivit me
25 Kwako wewe hutoka kiini cha sifa zangu katika kusanyiko kubwa, nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wakuchao wewe.
apud te laus mea in ecclesia magna vota mea reddam in conspectu timentium eum
26 Maskini watakula na kushiba, wale wamtafutao Bwana watamsifu: mioyo yenu na iishi milele!
edent pauperes et saturabuntur et laudabunt Dominum qui requirunt eum vivent corda eorum in saeculum saeculi
27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kumgeukia Bwana, nazo jamaa zote za mataifa watasujudu mbele zake,
reminiscentur et convertentur ad Dominum universi fines terrae et adorabunt in conspectu eius universae familiae gentium
28 kwa maana ufalme ni wa Bwana naye hutawala juu ya mataifa.
quoniam Dei est regnum et ipse dominabitur gentium
29 Matajiri wote wa dunia watasherehekea na kuabudu. Wote waendao mavumbini watapiga magoti mbele yake, wote ambao hawawezi kudumisha uhai wao.
manducaverunt et adoraverunt omnes pingues terrae in conspectu eius cadent omnes qui descendunt in terram
30 Wazao wa baadaye watamtumikia yeye; vizazi vijavyo vitajulishwa habari za Bwana.
et anima mea illi vivet et semen meum serviet ipsi
31 Watatangaza haki yake kwa watu ambao hawajazaliwa bado, kwa maana yeye ametenda hili.
adnuntiabitur Domino generatio ventura et adnuntiabunt iustitiam eius populo qui nascetur quem fecit Dominus