< Zaburi 22 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Kulungu wa Alfajiri.” Zaburi ya Daudi. Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa? Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu?
다윗의 시, 영장으로 아얠롓사할에 맞춘 노래 내 하나님이여 내 하나님이여 어찌 나를 버리셨나이까 어찌 나를 멀리하여 돕지 아니하옵시며 내 신음하는 소리를 듣지 아니하시나이까
2 Ee Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu, hata usiku, sinyamazi.
내 하나님이여 내가 낮에도 부르짖고 밤에도 잠잠치 아니하오나 응답지 아니하시나이다
3 Hata hivyo umesimikwa katika kiti cha enzi kama Uliye Mtakatifu; wewe ni sifa ya Israeli.
이스라엘의 찬송 중에 거하시는 주여 주는 거룩하시니이다
4 Kwako wewe baba zetu waliweka tumaini lao, walikutumaini nawe ukawaokoa.
우리 열조가 주께 의뢰하였고 의뢰하였으므로 저희를 건지셨나이다
5 Walikulilia wewe na ukawaokoa, walikutegemea wewe nao hawakuaibika.
저희가 주께 부르짖어 구원을 얻고 주께 의뢰하여 수치를 당치 아니하였나이다
6 Mimi ni mnyoo wala si mwanadamu, wanaume wamenibeza, na watu wamenidharau.
나는 벌레요 사람이 아니라 사람의 훼방거리요 백성의 조롱거리니이다
7 Wote wanionao hunidhihaki, hunivurumishia matusi, wakitikisa vichwa vyao:
나를 보는 자는 다 비웃으며 입술을 비쭉이고 머리를 흔들며 말하되
8 Husema, “Anamtegemea Bwana, basi Bwana na amwokoe. Amkomboe basi, kwa maana anapendezwa naye.”
저가 여호와께 의탁하니 구원하실걸, 저를 기뻐하시니 건지실걸 하나이다
9 Hata hivyo ulinitoa tumboni, ukanifanya nikutegemee, hata nilipokuwa ninanyonya matiti ya mama yangu.
오직 주께서 나를 모태에서 나오게 하시고 내 모친의 젖을 먹을 때에 의지하게 하셨나이다
10 Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa, toka tumboni mwa mama yangu umekuwa Mungu wangu.
내가 날 때부터 주께 맡긴바 되었고 모태에서 나올 때부터 주는 내 하나님이 되셨사오니
11 Usiwe mbali nami, kwa maana shida iko karibu na hakuna wa kunisaidia.
나를 멀리하지 마옵소서 환난이 가깝고 도울 자 없나이다
12 Mafahali wengi wamenizunguka, mafahali wa Bashani wenye nguvu wamenizingira.
많은 황소가 나를 에워싸며 바산의 힘센 소들이 나를 둘렀으며
13 Simba wangurumao wanaorarua mawindo yao hupanua vinywa vyao dhidi yangu.
내게 그 입을 벌림이 찢고 부르짖는 사자 같으니이다
14 Nimemiminwa kama maji, mifupa yangu yote imetoka katika viungo vyake. Moyo wangu umegeuka kuwa nta, umeyeyuka ndani yangu.
나는 물 같이 쏟아졌으며 내 모든 뼈는 어그러졌으며 내 마음은 촛밀 같아서 내 속에서 녹았으며
15 Nguvu zangu zimekauka kama kigae, ulimi wangu umegandamana na kaakaa la kinywa changu, kwa sababu umenilaza katika mavumbi ya kifo.
내 힘이 말라 질그릇 조각 같고 내 혀가 잇틀에 붙었나이다 주께서 또 나를 사망의 진토에 두셨나이다
16 Mbwa wamenizunguka, kundi la watu waovu limenizingira, wametoboa mikono yangu na miguu yangu.
개들이 나를 에워쌌으며 악한 무리가 나를 둘러 내 수족을 찔렀나이다
17 Naweza kuhesabu mifupa yangu yote, watu wananikodolea macho na kunisimanga.
내가 내 모든 뼈를 셀 수 있나이다 저희가 나를 주목하여 보고
18 Wanagawana nguo zangu wao kwa wao, na vazi langu wanalipigia kura.
내 겉옷을 나누며 속옷을 제비뽑나이다
19 Lakini wewe, Ee Bwana, usiwe mbali. Ee Nguvu yangu, uje haraka unisaidie.
여호와여 멀리하지 마옵소서 나의 힘이시여 속히 나를 도우소서
20 Okoa maisha yangu na upanga, uhai wangu wa thamani kutoka nguvu za mbwa.
내 영혼을 칼에서 건지시며 내 유일한 것을 개의 세력에서 구하소서
21 Niokoe kutoka kinywani mwa simba, niokoe kutoka pembe za mafahali mwitu.
나를 사자 입에서 구하소서 주께서 내게 응락하시고 들소 뿔에서 구원하셨나이다
22 Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu, katika kusanyiko nitakusifu wewe.
내가 주의 이름을 형제에게 선포하고 회중에서 주를 찬송하리이다
23 Ninyi ambao mnamcha Bwana, msifuni! Ninyi nyote wazao wote wa Yakobo, mheshimuni yeye! Mcheni yeye, ninyi wazao wote wa Israeli!
여호와를 두려워하는 너희여 그를 찬송할지어다 야곱의 모든 자손이여 그에게 영광을 돌릴지어다 너희 이스라엘 모든 자손이여 그를 경외할지어다
24 Kwa maana hakupuuza wala kudharau mateso ya aliyeonewa; hakumficha uso wake bali alisikiliza kilio chake ili amsaidie.
그는 곤고한 자의 곤고를 멸시하거나 싫어하지 아니하시며 그 얼굴을 저에게서 숨기지 아니하시고 부르짖을 때에 들으셨도다
25 Kwako wewe hutoka kiini cha sifa zangu katika kusanyiko kubwa, nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wakuchao wewe.
대회 중에 나의 찬송은 주께로서 온 것이니 주를 경외하는 자 앞에서 나의 서원을 갚으리이다
26 Maskini watakula na kushiba, wale wamtafutao Bwana watamsifu: mioyo yenu na iishi milele!
겸손한 자는 먹고 배부를 것이며 여호와를 찾는 자는 그를 찬송할 것이라 너희 마음은 영원히 살지어다
27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kumgeukia Bwana, nazo jamaa zote za mataifa watasujudu mbele zake,
땅의 모든 끝이 여호와를 기억하고 돌아오며 열방의 모든 족속이 주의 앞에 경배하리니
28 kwa maana ufalme ni wa Bwana naye hutawala juu ya mataifa.
나라는 여호와의 것이요 여호와는 열방의 주재심이로다
29 Matajiri wote wa dunia watasherehekea na kuabudu. Wote waendao mavumbini watapiga magoti mbele yake, wote ambao hawawezi kudumisha uhai wao.
세상의 모든 풍비한 자가 먹고 경배할 것이요 진토에 내려가는 자 곧 자기 영혼을 살리지 못할 자도 다 그 앞에 절하리로다
30 Wazao wa baadaye watamtumikia yeye; vizazi vijavyo vitajulishwa habari za Bwana.
후손이 그를 봉사할 것이요 대대에 주를 전할 것이며
31 Watatangaza haki yake kwa watu ambao hawajazaliwa bado, kwa maana yeye ametenda hili.
와서 그 공의를 장차 날 백성에게 전함이여 주께서 이를 행하셨다 할 것이로다

< Zaburi 22 >