< Zaburi 22 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Kulungu wa Alfajiri.” Zaburi ya Daudi. Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa? Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu?
あけぼのの鹿の調にあはせて伶長にうたはしめたるダビデの歌 わが神わが神なんぞ我をすてたまふや 何なれば遠くはなれて我をすくはず わが歎きのこゑをきき給はざるか
2 Ee Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu, hata usiku, sinyamazi.
ああわが神われ昼よばはれども汝こたへたまはず 夜よばはれどもわれ平安をえず
3 Hata hivyo umesimikwa katika kiti cha enzi kama Uliye Mtakatifu; wewe ni sifa ya Israeli.
然はあれイスラエルの讃美のなかに住たまふものよ汝はきよし
4 Kwako wewe baba zetu waliweka tumaini lao, walikutumaini nawe ukawaokoa.
われらの列祖はなんぢに依頼めり かれら依頼みたればこれを助けたまへり
5 Walikulilia wewe na ukawaokoa, walikutegemea wewe nao hawakuaibika.
かれら汝をよびて援をえ汝によりたのみて恥をおへることなかりき
6 Mimi ni mnyoo wala si mwanadamu, wanaume wamenibeza, na watu wamenidharau.
然はあれどわれは蟲にして人にあらず 世にそしられ民にいやしめらる
7 Wote wanionao hunidhihaki, hunivurumishia matusi, wakitikisa vichwa vyao:
すべてわれを見るものはわれをあざみわらひ 口唇をそらし首をふりていふ
8 Husema, “Anamtegemea Bwana, basi Bwana na amwokoe. Amkomboe basi, kwa maana anapendezwa naye.”
かれはヱホバによりたのめりヱホバ助くべし ヱホバかれを悦びたまふが故にたすくべしと
9 Hata hivyo ulinitoa tumboni, ukanifanya nikutegemee, hata nilipokuwa ninanyonya matiti ya mama yangu.
されど汝はわれを胎内よりいだし絵へるものなり わが母のふところにありしとき既になんぢに依頼ましめたまへり
10 Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa, toka tumboni mwa mama yangu umekuwa Mungu wangu.
我うまれいでしより汝にゆだねられたり わが母われを生しときより汝はわが神なり
11 Usiwe mbali nami, kwa maana shida iko karibu na hakuna wa kunisaidia.
われに遠ざかりたまふなかれ 患難ちかづき又すくふものなければなり
12 Mafahali wengi wamenizunguka, mafahali wa Bashani wenye nguvu wamenizingira.
おほくの牡牛われをめぐりバサンの力つよき牡牛われをかこめり
13 Simba wangurumao wanaorarua mawindo yao hupanua vinywa vyao dhidi yangu.
かれらは口をあけて我にむかひ物をかきさき吼うだく獅のごとし
14 Nimemiminwa kama maji, mifupa yangu yote imetoka katika viungo vyake. Moyo wangu umegeuka kuwa nta, umeyeyuka ndani yangu.
われ水のごとくそそぎいだされ わがもろもろの骨ははづれ わが心は蝋のごとくなりて腹のうちに鎔たり
15 Nguvu zangu zimekauka kama kigae, ulimi wangu umegandamana na kaakaa la kinywa changu, kwa sababu umenilaza katika mavumbi ya kifo.
わが力はかわきて陶器のくだけのごとく わが舌は齶にひたつけり なんぢわれを死の塵にふさせたまへり
16 Mbwa wamenizunguka, kundi la watu waovu limenizingira, wametoboa mikono yangu na miguu yangu.
そは犬われをめぐり惡きものの群われをかこみてわが手およびわが足をさしつらぬけり
17 Naweza kuhesabu mifupa yangu yote, watu wananikodolea macho na kunisimanga.
わが骨はことごとく數ふるばかりになりぬ 惡きものの目をとめて我をみる
18 Wanagawana nguo zangu wao kwa wao, na vazi langu wanalipigia kura.
かれらたがひにわが衣をわかち我がしたぎを鬮にす
19 Lakini wewe, Ee Bwana, usiwe mbali. Ee Nguvu yangu, uje haraka unisaidie.
ヱホバよ遠くはなれ居たまふなかれ わが力よねがはくは速きたりてわれを授けたまへ
20 Okoa maisha yangu na upanga, uhai wangu wa thamani kutoka nguvu za mbwa.
わがたましひを劍より助けいだし わが生命を犬のたけきいきほひより脱れしめたまへ
21 Niokoe kutoka kinywani mwa simba, niokoe kutoka pembe za mafahali mwitu.
われを獅の口また野牛のつのより救ひいだしたまへ なんぢ我にこたへたまへり
22 Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu, katika kusanyiko nitakusifu wewe.
われなんぢの名をわが兄弟にのべつたへ なんぢを會のなかにて讃たたへん
23 Ninyi ambao mnamcha Bwana, msifuni! Ninyi nyote wazao wote wa Yakobo, mheshimuni yeye! Mcheni yeye, ninyi wazao wote wa Israeli!
ヱホバを懼るるものよヱホバをほめたたへよ ヤコブのもろもろの裔よヱホバをあがめよ イスラエルのもろもろのすゑよヱホバを畏め
24 Kwa maana hakupuuza wala kudharau mateso ya aliyeonewa; hakumficha uso wake bali alisikiliza kilio chake ili amsaidie.
ヱホバはなやむものの辛苦をかろしめ棄たまはず これに聖顔をおほふことなくしてその叫ぶときにききたまへばなり
25 Kwako wewe hutoka kiini cha sifa zangu katika kusanyiko kubwa, nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wakuchao wewe.
大なる會のなかにてわが汝をほめたたふるは汝よりいづるなり わが誓ひしことはヱホバをおそるる者のまへにてことごとく償はん
26 Maskini watakula na kushiba, wale wamtafutao Bwana watamsifu: mioyo yenu na iishi milele!
謙遜者はくらひて飽ことをえ ヱホバをたづねもとむるものはヱホバをほめたたへん 願くはなんぢらの心とこしへに生んことを
27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kumgeukia Bwana, nazo jamaa zote za mataifa watasujudu mbele zake,
地のはては皆おもひいだしてヱホバに歸りもろもろの國の族はみな前にふしをがむべし
28 kwa maana ufalme ni wa Bwana naye hutawala juu ya mataifa.
國はヱホバのものなればなり ヱホバはもろもろの國人をすべをさめたまふ
29 Matajiri wote wa dunia watasherehekea na kuabudu. Wote waendao mavumbini watapiga magoti mbele yake, wote ambao hawawezi kudumisha uhai wao.
地のこえたるものは皆くらひてヱホバををがみ塵にくたるものと己がたましひを存ふること能はざるものと皆そのみまへに拝脆かん
30 Wazao wa baadaye watamtumikia yeye; vizazi vijavyo vitajulishwa habari za Bwana.
たみの裔のうちにヱホバにつかる者あらん 主のことは代々にかたりつたへらるべし
31 Watatangaza haki yake kwa watu ambao hawajazaliwa bado, kwa maana yeye ametenda hili.
かれら來りて此はヱホバの行爲なりとてその義を後にうまるる民にのべつたへん

< Zaburi 22 >