< Zaburi 22 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Kulungu wa Alfajiri.” Zaburi ya Daudi. Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa? Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu?
Pour la fin, pour le secours du matin, psaume de David. Dieu, mon Dieu, regardez-moi: pourquoi m’avez-vous délaissé? Les paroles de mes péchés sont loin de mon salut.
2 Ee Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu, hata usiku, sinyamazi.
Mon Dieu, je crierai pendant le jour, et vous ne m’exaucerez pas: et pendant la nuit, et ce n’est point à moi une folie.
3 Hata hivyo umesimikwa katika kiti cha enzi kama Uliye Mtakatifu; wewe ni sifa ya Israeli.
Mais vous, vous habitez dans un sanctuaire, vous la louange d’Israël.
4 Kwako wewe baba zetu waliweka tumaini lao, walikutumaini nawe ukawaokoa.
C’est en vous qu’ont espéré nos pères: ils ont espéré, et vous les avez délivrés.
5 Walikulilia wewe na ukawaokoa, walikutegemea wewe nao hawakuaibika.
Vers vous ils ont crié et ils ont été sauvés: en vous ils ont espéré, et ils n’ont point été confondus.
6 Mimi ni mnyoo wala si mwanadamu, wanaume wamenibeza, na watu wamenidharau.
Pour moi je suis un ver et non pas un homme; l’opprobre des hommes et l’abjection du peuple.
7 Wote wanionao hunidhihaki, hunivurumishia matusi, wakitikisa vichwa vyao:
Tout ceux qui m’ont vu m’ont tourné en dérision: ils ont parlé du bout des lèvres, et ils ont secoué la tête.
8 Husema, “Anamtegemea Bwana, basi Bwana na amwokoe. Amkomboe basi, kwa maana anapendezwa naye.”
Il a espéré dans le Seigneur, qu’il le délivre; qu’il le sauve, puisqu’il l’aime.
9 Hata hivyo ulinitoa tumboni, ukanifanya nikutegemee, hata nilipokuwa ninanyonya matiti ya mama yangu.
Cependant c’est vous qui m’avez tiré du sein de ma mère: vous êtes mon espérance depuis que je suçais les mamelles de ma mère.
10 Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa, toka tumboni mwa mama yangu umekuwa Mungu wangu.
C’est sur vous que j’ai été posé, en sortant de son sein; depuis que j’étais dans les entrailles de ma mère, vous êtes mon Dieu.
11 Usiwe mbali nami, kwa maana shida iko karibu na hakuna wa kunisaidia.
Ne vous éloignez pas de moi:
12 Mafahali wengi wamenizunguka, mafahali wa Bashani wenye nguvu wamenizingira.
De jeunes taureaux en grand nombre m’ont environné; des taureaux gras m’ont assiégé.
13 Simba wangurumao wanaorarua mawindo yao hupanua vinywa vyao dhidi yangu.
Ils ont ouvert sur moi leur gueule comme un lion ravissant et rugissant.
14 Nimemiminwa kama maji, mifupa yangu yote imetoka katika viungo vyake. Moyo wangu umegeuka kuwa nta, umeyeyuka ndani yangu.
Je me suis épanché comme de l’eau, et tous mes os se sont déboîtés. Mon cœur est devenu au dedans de moi comme une cire qui se fond.
15 Nguvu zangu zimekauka kama kigae, ulimi wangu umegandamana na kaakaa la kinywa changu, kwa sababu umenilaza katika mavumbi ya kifo.
Ma force s’est desséchée comme un têt, et ma langue s’est attachée à mon palais; et vous m’avez conduit à la poussière de la mort.
16 Mbwa wamenizunguka, kundi la watu waovu limenizingira, wametoboa mikono yangu na miguu yangu.
Parce que des chiens nombreux m’ont environné; un conseil de méchants m’a assiégé: Ils ont percé mes mains et mes pieds:
17 Naweza kuhesabu mifupa yangu yote, watu wananikodolea macho na kunisimanga.
Ils ont compté tous mes os. Ils m’ont eux-mêmes considéré et regardé attentivement.
18 Wanagawana nguo zangu wao kwa wao, na vazi langu wanalipigia kura.
Ils se sont partagé mes vêtements, et sur ma robe ils ont jeté le sort.
19 Lakini wewe, Ee Bwana, usiwe mbali. Ee Nguvu yangu, uje haraka unisaidie.
Mais vous, Seigneur, n’éloignez pas votre secours de moi: voyez à ma défense.
20 Okoa maisha yangu na upanga, uhai wangu wa thamani kutoka nguvu za mbwa.
Arrachez mon âme à l’épée à double tranchant; et mon unique de la main du chien.
21 Niokoe kutoka kinywani mwa simba, niokoe kutoka pembe za mafahali mwitu.
Sauvez-moi de la gueule du lion; et ma faiblesse des cornes des licornes.
22 Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu, katika kusanyiko nitakusifu wewe.
Je raconterai votre nom à mes frères; je vous louerai au milieu de l’assemblée.
23 Ninyi ambao mnamcha Bwana, msifuni! Ninyi nyote wazao wote wa Yakobo, mheshimuni yeye! Mcheni yeye, ninyi wazao wote wa Israeli!
Vous qui craignez le Seigneur, louez-le; race entière de Jacob, glorifiez-le:
24 Kwa maana hakupuuza wala kudharau mateso ya aliyeonewa; hakumficha uso wake bali alisikiliza kilio chake ili amsaidie.
Que toute la race d’Israël le craigne, parce qu’il n’a pas méprisé ni dédaigné la supplication du pauvre; Et qu’il n’a point détourné sa face de moi, et que lorsque je criais vers lui, il m’a exaucé.
25 Kwako wewe hutoka kiini cha sifa zangu katika kusanyiko kubwa, nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wakuchao wewe.
Devant vous sera ma louange dans une grande assemblée: je rendrai mes vœux en présence de ceux qui le craignent.
26 Maskini watakula na kushiba, wale wamtafutao Bwana watamsifu: mioyo yenu na iishi milele!
Les pauvres mangeront et seront rassasiés; et ils loueront le Seigneur, ceux qui le recherchent; leurs cœurs vivront dans les siècles des siècles.
27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kumgeukia Bwana, nazo jamaa zote za mataifa watasujudu mbele zake,
Tous les confins de la terre se souviendront du Seigneur et se convertiront à lui: Et toutes les familles des nations adoreront en sa présence.
28 kwa maana ufalme ni wa Bwana naye hutawala juu ya mataifa.
Parce qu’au Seigneur appartient le règne; et que c’est lui qui dominera sur les nations.
29 Matajiri wote wa dunia watasherehekea na kuabudu. Wote waendao mavumbini watapiga magoti mbele yake, wote ambao hawawezi kudumisha uhai wao.
Tous les riches de la terre ont mangé et ont adoré: en sa présence tomberont tous ceux qui descendent dans la terre.
30 Wazao wa baadaye watamtumikia yeye; vizazi vijavyo vitajulishwa habari za Bwana.
Et mon âme vivra pour lui; et ma postérité le servira.
31 Watatangaza haki yake kwa watu ambao hawajazaliwa bado, kwa maana yeye ametenda hili.
La génération qui doit venir sera annoncée au Seigneur; et les cieux annonceront sa justice au peuple qui naîtra, et qu’a fait le Seigneur.

< Zaburi 22 >