< Zaburi 22 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Kulungu wa Alfajiri.” Zaburi ya Daudi. Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa? Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu?
Au maître de chant. Sur « Biche de l’aurore ». Psaume de David. Mon Dieu, mon Dieu, pourquoi m’as-tu abandonné? Je gémis, et le salut reste loin de moi!
2 Ee Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu, hata usiku, sinyamazi.
Mon Dieu, je crie pendant le jour, et tu ne réponds pas; la nuit, et je n’ai point de repos.
3 Hata hivyo umesimikwa katika kiti cha enzi kama Uliye Mtakatifu; wewe ni sifa ya Israeli.
Pourtant tu es saint, tu habites parmi les hymnes d’Israël.
4 Kwako wewe baba zetu waliweka tumaini lao, walikutumaini nawe ukawaokoa.
En toi se sont confiés nos pères; ils se sont confiés, et tu les as délivrés.
5 Walikulilia wewe na ukawaokoa, walikutegemea wewe nao hawakuaibika.
Ils ont crié vers toi, et ils ont été sauvés; ils se sont confiés en toi, et ils n’ont pas été confus.
6 Mimi ni mnyoo wala si mwanadamu, wanaume wamenibeza, na watu wamenidharau.
Et moi, je suis un ver, et non un homme, l’opprobre des hommes et le rebut du peuple.
7 Wote wanionao hunidhihaki, hunivurumishia matusi, wakitikisa vichwa vyao:
Tous ceux qui me voient se moquent de moi; ils ouvrent les lèvres, ils branlent la tête:
8 Husema, “Anamtegemea Bwana, basi Bwana na amwokoe. Amkomboe basi, kwa maana anapendezwa naye.”
« Qu’il s’abandonne à Yahweh! Qu’il le sauve, qu’il le délivre, puisqu’il l’aime! »
9 Hata hivyo ulinitoa tumboni, ukanifanya nikutegemee, hata nilipokuwa ninanyonya matiti ya mama yangu.
Oui, c’est toi qui m’as tiré du sein maternel, qui m’as donné confiance sur les mamelles de ma mère.
10 Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa, toka tumboni mwa mama yangu umekuwa Mungu wangu.
Dès ma naissance, je t’ai été abandonné; depuis le sein de ma mère, c’est toi qui es mon Dieu.
11 Usiwe mbali nami, kwa maana shida iko karibu na hakuna wa kunisaidia.
Ne t’éloigne pas de moi, car l’angoisse est proche, car personne ne vient à mon secours.
12 Mafahali wengi wamenizunguka, mafahali wa Bashani wenye nguvu wamenizingira.
Autour de moi sont de nombreux taureaux, les forts de Basan m’environnent.
13 Simba wangurumao wanaorarua mawindo yao hupanua vinywa vyao dhidi yangu.
Ils ouvrent contre moi leur gueule, comme un lion qui déchire et rugit.
14 Nimemiminwa kama maji, mifupa yangu yote imetoka katika viungo vyake. Moyo wangu umegeuka kuwa nta, umeyeyuka ndani yangu.
Je suis comme de l’eau qui s’écoule, et tous mes os sont disjoints; mon cœur est comme de la cire, il se fond dans mes entrailles.
15 Nguvu zangu zimekauka kama kigae, ulimi wangu umegandamana na kaakaa la kinywa changu, kwa sababu umenilaza katika mavumbi ya kifo.
Ma force s’est desséchée comme un tesson d’argile, et ma langue s’attache à mon palais; tu me couches dans la poussière de la mort.
16 Mbwa wamenizunguka, kundi la watu waovu limenizingira, wametoboa mikono yangu na miguu yangu.
Car des chiens m’environnent, une troupe de scélérats rôdent autour de moi; ils ont percé mes pieds et mes mains,
17 Naweza kuhesabu mifupa yangu yote, watu wananikodolea macho na kunisimanga.
je pourrais compter tous mes os. Eux, ils m’observent, ils me contemplent;
18 Wanagawana nguo zangu wao kwa wao, na vazi langu wanalipigia kura.
ils se partagent mes vêtements, ils tirent au sort ma tunique.
19 Lakini wewe, Ee Bwana, usiwe mbali. Ee Nguvu yangu, uje haraka unisaidie.
Et toi, Yahweh, ne t’éloigne pas! Toi qui es ma force, viens en hâte à mon secours!
20 Okoa maisha yangu na upanga, uhai wangu wa thamani kutoka nguvu za mbwa.
Délivre mon âme de l’épée, ma vie du pouvoir du chien!
21 Niokoe kutoka kinywani mwa simba, niokoe kutoka pembe za mafahali mwitu.
Sauve-moi de la gueule du lion, tire-moi des cornes du buffle!
22 Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu, katika kusanyiko nitakusifu wewe.
Alors j’annoncerai ton nom à mes frères, au milieu de l’assemblée je te louerai:
23 Ninyi ambao mnamcha Bwana, msifuni! Ninyi nyote wazao wote wa Yakobo, mheshimuni yeye! Mcheni yeye, ninyi wazao wote wa Israeli!
« Vous qui craignez Yahweh, louez-le! Vous tous, postérité de Jacob, glorifiez-le! Révérez-le, vous tous, postérité d’Israël!
24 Kwa maana hakupuuza wala kudharau mateso ya aliyeonewa; hakumficha uso wake bali alisikiliza kilio chake ili amsaidie.
Car il n’a pas méprisé, il n’a pas rejeté la souffrance de l’affligé, il n’a pas caché sa face devant lui, et quand l’affligé a crié vers lui, il a entendu. »
25 Kwako wewe hutoka kiini cha sifa zangu katika kusanyiko kubwa, nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wakuchao wewe.
Grâce à toi, mon hymne retentira dans la grande assemblée, j’acquitterai mes vœux en présence de ceux qui te craignent.
26 Maskini watakula na kushiba, wale wamtafutao Bwana watamsifu: mioyo yenu na iishi milele!
Les affligés mangeront et se rassasieront; ceux qui cherchent Yahweh le loueront. Que votre cœur revive à jamais!
27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kumgeukia Bwana, nazo jamaa zote za mataifa watasujudu mbele zake,
Toutes les extrémités de la terre se souviendront et se tourneront vers Yahweh, et toutes les familles des nations se prosterneront devant sa face.
28 kwa maana ufalme ni wa Bwana naye hutawala juu ya mataifa.
Car à Yahweh appartient l’empire, il domine sur les nations.
29 Matajiri wote wa dunia watasherehekea na kuabudu. Wote waendao mavumbini watapiga magoti mbele yake, wote ambao hawawezi kudumisha uhai wao.
Les puissants de la terre mangeront et se prosterneront; devant lui s’inclineront tous ceux qui descendent à la poussière, ceux qui ne peuvent prolonger leur vie.
30 Wazao wa baadaye watamtumikia yeye; vizazi vijavyo vitajulishwa habari za Bwana.
La postérité le servira; on parlera du Seigneur à la génération future.
31 Watatangaza haki yake kwa watu ambao hawajazaliwa bado, kwa maana yeye ametenda hili.
Ils viendront et ils annonceront sa justice, au peuple qui naîtra, ils diront ce qu’il a fait.