< Zaburi 22 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Kulungu wa Alfajiri.” Zaburi ya Daudi. Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa? Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu?
Pour le chef musicien; réglé sur « The Dœ of the Morning ». Un psaume de David. Mon Dieu, mon Dieu, pourquoi m'as-tu abandonné? Pourquoi es-tu si loin de me secourir, et des paroles de mes gémissements?
2 Ee Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu, hata usiku, sinyamazi.
Mon Dieu, je crie pendant le jour, mais tu ne réponds pas; dans la saison de la nuit, et je ne suis pas silencieux.
3 Hata hivyo umesimikwa katika kiti cha enzi kama Uliye Mtakatifu; wewe ni sifa ya Israeli.
Mais toi, tu es saint, vous qui habitez les louanges d'Israël.
4 Kwako wewe baba zetu waliweka tumaini lao, walikutumaini nawe ukawaokoa.
Nos pères avaient confiance en toi. Ils ont fait confiance, et vous les avez délivrés.
5 Walikulilia wewe na ukawaokoa, walikutegemea wewe nao hawakuaibika.
Ils ont crié vers toi, et ils ont été délivrés. Ils ont eu confiance en vous, et n'ont pas été déçus.
6 Mimi ni mnyoo wala si mwanadamu, wanaume wamenibeza, na watu wamenidharau.
Mais moi, je suis un ver, et je ne suis pas un homme; un opprobre des hommes, et méprisé par le peuple.
7 Wote wanionao hunidhihaki, hunivurumishia matusi, wakitikisa vichwa vyao:
Tous ceux qui me voient se moquent de moi. Ils m'insultent de leurs lèvres. Ils secouent la tête en disant,
8 Husema, “Anamtegemea Bwana, basi Bwana na amwokoe. Amkomboe basi, kwa maana anapendezwa naye.”
« Il se confie en Yahvé. Laissez-le le délivrer. Qu'il le sauve, puisqu'il se complaît en lui. »
9 Hata hivyo ulinitoa tumboni, ukanifanya nikutegemee, hata nilipokuwa ninanyonya matiti ya mama yangu.
Mais c'est toi qui m'as fait sortir du ventre de ma mère. Tu m'as fait confiance alors que j'étais aux seins de ma mère.
10 Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa, toka tumboni mwa mama yangu umekuwa Mungu wangu.
J'ai été jeté sur toi dès le sein de ma mère. Tu es mon Dieu depuis que ma mère m'a porté.
11 Usiwe mbali nami, kwa maana shida iko karibu na hakuna wa kunisaidia.
Ne t'éloigne pas de moi, car le malheur est proche. Car il n'y a personne pour aider.
12 Mafahali wengi wamenizunguka, mafahali wa Bashani wenye nguvu wamenizingira.
De nombreux taureaux m'ont entouré. De puissants taureaux de Bashan m'ont encerclé.
13 Simba wangurumao wanaorarua mawindo yao hupanua vinywa vyao dhidi yangu.
Ils ouvrent largement la bouche contre moi, des lions déchirant leur proie et rugissant.
14 Nimemiminwa kama maji, mifupa yangu yote imetoka katika viungo vyake. Moyo wangu umegeuka kuwa nta, umeyeyuka ndani yangu.
Je suis répandu comme de l'eau. Tous mes os sont déréglés. Mon cœur est comme de la cire. Il est fondu en moi.
15 Nguvu zangu zimekauka kama kigae, ulimi wangu umegandamana na kaakaa la kinywa changu, kwa sababu umenilaza katika mavumbi ya kifo.
Ma force est desséchée comme un pot de fleurs. Ma langue se colle au palais. Tu m'as amené dans la poussière de la mort.
16 Mbwa wamenizunguka, kundi la watu waovu limenizingira, wametoboa mikono yangu na miguu yangu.
Car les chiens m'ont entouré. Une troupe de malfaiteurs m'a enfermé. Ils ont percé mes mains et mes pieds.
17 Naweza kuhesabu mifupa yangu yote, watu wananikodolea macho na kunisimanga.
Je peux compter tous mes os. Ils me regardent et me fixent.
18 Wanagawana nguo zangu wao kwa wao, na vazi langu wanalipigia kura.
Ils partagent mes vêtements entre eux. Ils ont tiré au sort mes vêtements.
19 Lakini wewe, Ee Bwana, usiwe mbali. Ee Nguvu yangu, uje haraka unisaidie.
Mais ne t'éloigne pas, Yahvé. Vous êtes mon aide. Dépêchez-vous de m'aider!
20 Okoa maisha yangu na upanga, uhai wangu wa thamani kutoka nguvu za mbwa.
Délivre mon âme de l'épée, ma précieuse vie du pouvoir du chien.
21 Niokoe kutoka kinywani mwa simba, niokoe kutoka pembe za mafahali mwitu.
Sauve-moi de la gueule du lion! Oui, tu m'as sauvé des cornes des bœufs sauvages.
22 Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu, katika kusanyiko nitakusifu wewe.
Je proclamerai ton nom à mes frères. Au milieu de l'assemblée, je te louerai.
23 Ninyi ambao mnamcha Bwana, msifuni! Ninyi nyote wazao wote wa Yakobo, mheshimuni yeye! Mcheni yeye, ninyi wazao wote wa Israeli!
Vous qui craignez Yahvé, louez-le! Vous tous, descendants de Jacob, glorifiez-le! Restez en admiration devant lui, vous tous, descendants d'Israël!
24 Kwa maana hakupuuza wala kudharau mateso ya aliyeonewa; hakumficha uso wake bali alisikiliza kilio chake ili amsaidie.
Car il n'a pas méprisé ni abhorré l'affliction des affligés, Il ne lui a pas non plus caché son visage; mais quand il a crié vers lui, il a entendu.
25 Kwako wewe hutoka kiini cha sifa zangu katika kusanyiko kubwa, nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wakuchao wewe.
Je te loue dans la grande assemblée. J'accomplirai mes vœux devant ceux qui le craignent.
26 Maskini watakula na kushiba, wale wamtafutao Bwana watamsifu: mioyo yenu na iishi milele!
Les humbles mangeront et seront rassasiés. Ceux qui le cherchent loueront Yahvé. Que vos cœurs vivent à jamais.
27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kumgeukia Bwana, nazo jamaa zote za mataifa watasujudu mbele zake,
Toutes les extrémités de la terre se souviendront et se tourneront vers Yahvé. Tous les parents des nations se prosterneront devant toi.
28 kwa maana ufalme ni wa Bwana naye hutawala juu ya mataifa.
Car le royaume appartient à Yahvé. Il est le chef des nations.
29 Matajiri wote wa dunia watasherehekea na kuabudu. Wote waendao mavumbini watapiga magoti mbele yake, wote ambao hawawezi kudumisha uhai wao.
Tous les riches de la terre mangeront et se prosterneront. Tous ceux qui descendent dans la poussière s'inclineront devant lui, même celui qui ne peut pas garder son âme en vie.
30 Wazao wa baadaye watamtumikia yeye; vizazi vijavyo vitajulishwa habari za Bwana.
La postérité le servira. On parlera du Seigneur aux générations futures.
31 Watatangaza haki yake kwa watu ambao hawajazaliwa bado, kwa maana yeye ametenda hili.
Ils viendront et annonceront sa justice à un peuple qui naîtra, car il l'a fait.

< Zaburi 22 >