< Zaburi 22 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Kulungu wa Alfajiri.” Zaburi ya Daudi. Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa? Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu?
To the choirmaster on [the] doe of the dawn a psalm of David. O God my God my why? have you forsaken me [are] far from deliverance my [the] words of cry of distress my.
2 Ee Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu, hata usiku, sinyamazi.
O God my I call out by day and not you answer and night and not repose [belongs] to me.
3 Hata hivyo umesimikwa katika kiti cha enzi kama Uliye Mtakatifu; wewe ni sifa ya Israeli.
And you [are] holy sitting [the] praises of Israel.
4 Kwako wewe baba zetu waliweka tumaini lao, walikutumaini nawe ukawaokoa.
In you they trusted ancestors our they trusted and you delivered them.
5 Walikulilia wewe na ukawaokoa, walikutegemea wewe nao hawakuaibika.
To you they cried out and they were delivered in you they trusted and not they were ashamed.
6 Mimi ni mnyoo wala si mwanadamu, wanaume wamenibeza, na watu wamenidharau.
And I [am] a worm and not a man a reproach of humankind and despised of a people.
7 Wote wanionao hunidhihaki, hunivurumishia matusi, wakitikisa vichwa vyao:
All [those who] see me they mock me they make a separation with a lip they shake a head.
8 Husema, “Anamtegemea Bwana, basi Bwana na amwokoe. Amkomboe basi, kwa maana anapendezwa naye.”
Roll to Yahweh let him rescue him let him deliver him for he delights in him.
9 Hata hivyo ulinitoa tumboni, ukanifanya nikutegemee, hata nilipokuwa ninanyonya matiti ya mama yangu.
For you [were] drawing forth me from [the] belly [were] making trust me on [the] breasts of mother my.
10 Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa, toka tumboni mwa mama yangu umekuwa Mungu wangu.
On you I was cast from [the] womb from [the] belly of mother my [have been] God my you.
11 Usiwe mbali nami, kwa maana shida iko karibu na hakuna wa kunisaidia.
May not you be far from me for trouble [is] near for there not [is] a helper.
12 Mafahali wengi wamenizunguka, mafahali wa Bashani wenye nguvu wamenizingira.
They have surrounded me bulls many mighty [bulls] of Bashan they have encircled me.
13 Simba wangurumao wanaorarua mawindo yao hupanua vinywa vyao dhidi yangu.
They have opened on me mouth their a lion tearing and roaring.
14 Nimemiminwa kama maji, mifupa yangu yote imetoka katika viungo vyake. Moyo wangu umegeuka kuwa nta, umeyeyuka ndani yangu.
Like water I have been poured out and they have become dislocated all bones my it has become heart my like wax it has melted in [the] midst of inward parts my.
15 Nguvu zangu zimekauka kama kigae, ulimi wangu umegandamana na kaakaa la kinywa changu, kwa sababu umenilaza katika mavumbi ya kifo.
It has dried up like earthenware - strength my and tongue my [has been] made to cling to jaws my and to [the] dust of death you put me.
16 Mbwa wamenizunguka, kundi la watu waovu limenizingira, wametoboa mikono yangu na miguu yangu.
For they have surrounded me dogs a company of evil-doers they have encircled me (like a lion *L(D)*) hands my and feet my.
17 Naweza kuhesabu mifupa yangu yote, watu wananikodolea macho na kunisimanga.
I count all bones my they they look they look on me.
18 Wanagawana nguo zangu wao kwa wao, na vazi langu wanalipigia kura.
They distribute clothes my to themselves and on clothing my they cast a lot.
19 Lakini wewe, Ee Bwana, usiwe mbali. Ee Nguvu yangu, uje haraka unisaidie.
And you O Yahweh may not you be distant O strength my to help my make haste!
20 Okoa maisha yangu na upanga, uhai wangu wa thamani kutoka nguvu za mbwa.
Deliver! from [the] sword life my from [the] hand of a dog only [life] my.
21 Niokoe kutoka kinywani mwa simba, niokoe kutoka pembe za mafahali mwitu.
Save me from [the] mouth of a lion and from [the] horns of wild oxen you have answered me.
22 Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu, katika kusanyiko nitakusifu wewe.
I will recount name your to brothers my in among [the] assembly I will praise you.
23 Ninyi ambao mnamcha Bwana, msifuni! Ninyi nyote wazao wote wa Yakobo, mheshimuni yeye! Mcheni yeye, ninyi wazao wote wa Israeli!
O [those] fearing Yahweh - praise him O all [the] offspring of Jacob honor him and be afraid from him O all [the] offspring of Israel.
24 Kwa maana hakupuuza wala kudharau mateso ya aliyeonewa; hakumficha uso wake bali alisikiliza kilio chake ili amsaidie.
For not he has despised and not he has detested [the] affliction of an afflicted [person] and not he has hidden face his from him and when cried for help he to him he heard.
25 Kwako wewe hutoka kiini cha sifa zangu katika kusanyiko kubwa, nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wakuchao wewe.
[is] from With you praise my in [the] assembly great vows my I will pay before [those] fearing him.
26 Maskini watakula na kushiba, wale wamtafutao Bwana watamsifu: mioyo yenu na iishi milele!
They will eat humble [people] - so they may be satisfied they will praise Yahweh [those who] seek him may it live heart your for ever.
27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kumgeukia Bwana, nazo jamaa zote za mataifa watasujudu mbele zake,
They will remember - and they may turn to Yahweh all [the] ends of [the] earth so they may bow down before you all [the] clans of [the] nations.
28 kwa maana ufalme ni wa Bwana naye hutawala juu ya mataifa.
For [belongs] to Yahweh the kingship and [he is] ruling over the nations.
29 Matajiri wote wa dunia watasherehekea na kuabudu. Wote waendao mavumbini watapiga magoti mbele yake, wote ambao hawawezi kudumisha uhai wao.
They have eaten and they have bowed down - all [the] fat [people] of [the] earth before him they will bow down all [those who are] about to go down of dust and life his not he has preserved alive.
30 Wazao wa baadaye watamtumikia yeye; vizazi vijavyo vitajulishwa habari za Bwana.
Offspring it will serve him it will be recounted of [the] Lord to the generation.
31 Watatangaza haki yake kwa watu ambao hawajazaliwa bado, kwa maana yeye ametenda hili.
They will come and they may declare righteousness his to a people about to be born that he has acted.

< Zaburi 22 >